• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

ZAIDI YA WAZEE 2000 WAPATA KADI ZA BIMA YA AFYA

Imewekwa: May 12th, 2018

Imeandaliwa na; Aisha Bakari - TangaTV

Jumla ya Wazee 2703 wa Jiji la Tanga wamepatiwa kadi za bima ya afya ya jamii (CHF) leo. Zoezi la kugawa kadi hizo ambazo zimegusa kaya 1604, limefanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Tanga Jiji, liliongozwa na Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Akiongea kwenye zoezi hilo, Mhe Ummy aliwasifia Jiji la Tanga kwa kuwapa vitambulisho na kuwalipia wazee bima ya afya. “Tanga, nyie mmejiongeza, maana hamkuwapa wazee vitambulisho tuu, bali na kuwalipia kabisa bima ya afya ili kuweza kupata huduma za afya bila ya malipo, Kaimu Meya na Kaimu Mkurugenzi hongereni sana na kwa hakika Tanga hamjaniangusha.” Alisema kwa kusifia na kutoa pongezi.

Akiongeza juu ya kuwalipia wazee kadi ya bima ya afya, Mhe Ummy alisema ya kwamba Jiji la Tanga linaunga na Halmashauri ya Mji wa Kahama kuwa halmashauri pekee zinazowalipia wazee huduma ya afya, hakika wametekeleza maelekezo ya serikali kwa ukamifu. “Kwa kuwa na kadi ya bima ya afya kunamfanya mzee huyu kupata huduma zote za afya bure na bila ya kuwa na ule usumbufu wa kwenda kwa Mtandaji wa Kata na Mtendaji wa Mtaa ili aandikiwe barua”

Wakiongea na mwandishi wa habari hii, baadhi ya wazee waliopata kadi ya bima ya afya, waliishukuru Serikali kwa kuwaangalia kwa jicho la huruma na hakika wanaona Serikali yao bado inawajali na kuwathamini. “Mjukuu wangu, kwa umri wetu huu magonjwa ndio nyumbani kwake, sasa kama huna pesa na huna namna ya kupata matibabu hapo inakuwa mtihani. Japo suala la kufa ni ahadi ya Mwenyezi Mungu lakini kukosa matibabu kunachangia vifo vya haraka kwetu sisi wazee” alisema mmoja ya wazee hao.

Kuwapatia wazee huduma za afya bure ni agizo lilitolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kupitia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kupitia agizo hilo Halmashauri zinatakiwa kuwapa wazee vitambulisho vya matibabu bure wazee wote wasio na uwezo ili kuwaondoshea usumbufu wanapokwenda hospitali kutibiwa.

Baadhi ya wazee wakimsikiliza Mhe Ummy


Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.