• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

NANE NANE 2025 KANDA YA MASHARIKI: TANGA JIJI YAJIPANGA KUONYESHA UTEKELEZAJI WA ILANI..

Imewekwa: July 20th, 2025

Julai 8, 2025.

Morogoro.

Maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi maarufu kama nane nane, yanayofanyika kuanzia Augosti 01 - 08, kila mwaka, kwa mwaka huu wa 2025, yanafanyika ikiwa pia nchi inaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Uchaguzi mkuu, kwa mujibu wa katiba yetu, hufanyika kila baada ya miaka mitano. Na wakati wa uchaguzi mkuu, vyama hutoa "Ilani zao za uchaguzi" ambazo ni ahadi au mipango ya chama kwa wananchi iwapo kitashika dola, na chama chenye ilani nzuri, wananchi hukichagua kuongoza nchi.


Maonesho ya nane nane, hufanyika kwa kanda. Moja ya kanda hizo, ni kanda ya Mashariki, inayojumuisha Mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es Salaam na Tanga, na hufanyika katika Uwanja wa maonesho wa Mwl. J. K. Nyerere, uliopo Manispaa ya Morogoro. Maonesho hayo kwa mwaka huu, 2025, yanabeba kauli mbiu isemayo “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025"


Halmashauri ya Jiji la Tanga ni moja ya Halmashauri zinazounda kanda hiyo, na mwaka huu, imejipanga kushiriki maonesho hayo kwa kuonyesha kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuleta mapinduzi kwenye kilimo, ufugaji na uvuvi.


Halmashauri ya Jiji la Tanga imefanikiwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama tawala (Chama cha Mapinduzi) katika maeneo tofauti, ikiwa ni pamoja na hili la kilimo, mifugo na uvuvi. Mafanikio haya ambayo yatawasilishwa kwa takwimu katika nane nane mwaka huu, kwenye banda la maonesho la Jiji la Tanga, yataonyesha hali ilivyokuwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita, na mafanikio yaliyofikiwa sasa, na kuwawezesha wakulima, wafugaji na wavuvi kujenga uchumi wao na ustawi wa taifa.


Katika banda hilo, wananchi wataweza kuona namna Halmashauri ilivyotekeleza lengo la kukifanya kilimo kinakuwa cha kisasa na cha kibiashara, ili kuhakikisha kuwa Taifa linajitosheleza kwa chakula, kuimarisha uchumi, kuongeza kipato cha wakulima, kuwa kichocheo cha kukua kwa viwanda na kuongeza ajira.


Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Mhandisi Juma Hamsini, amewaalika watu wote watakao weza kufika katika uwanja wa maonesho wa Mwl. J. K. Nyerere, Manispaa ya Morogoro, kufika katika banda la Jiji la Tanga kuweza kujionea mapinduzi hayo makubwa ya kilimo, ufugaji na uchumi wa bluu yatakayowasilishwa na wataalamu wa Halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JIJI LA TANGA AKABIDHI GARI NNE MPYA KWA IDARA NA VITENGO..

    July 22, 2025
  • LACI YATAMBULISHA MRADI TANGA JIJI..

    July 20, 2025
  • MAKUBWA MAWILI TUKIUANZA MWAKA 2025/2026..

    July 20, 2025
  • NANE NANE 2025 KANDA YA MASHARIKI: TANGA JIJI YAJIPANGA KUONYESHA UTEKELEZAJI WA ILANI..

    July 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.