• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

ZAIDI YA SHILLINGI BILLION MOJA KUJENGA MLANGO WA CHUMA

Imewekwa: July 27th, 2022

ZAIDI YA SHILLINGI BILLION MOJA KUJENGA MLANGO WA CHUMA

Na: Mussa Labani

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Jiji la Tanga

Soko maarufu la Mlango wa Chuma lililopo kata ya Majengo Jijini Tanga, linatarajiwa kufanyiwa ukarabati mkubwa utakaoligeuza soko hilo kuwa la kisasa lenye mandhari ya kuvutia na kuwezesha upatikanaji wa huduma zote muhimu katika masoko.

Akitoa taarifa ya hatua za maandalizi ya ukarabati huo, kwa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya ya Baraza la Madiwani wa Jiji la Tanga, Mchumi wa Jiji la Tanga, Bwana Simeon Vedastus Mzee ameieleza Kamati hiyo kuwa, tayari kiasi cha shillingi million 100 zimekwisha tolewa kwa kazi hiyo, na shillingi million 150 zimetengwa ili kufanya jumla ya shillingi million 250 kama fedha za awali huku mradi mzima ukitarajiwa kugharimu kiasi cha zaidi ya shillingi Billion moja.

Kwasasa taratibu zinafanyika za kuwahamisha kwa muda wafanyabiashara wa soko hilo ili kupisha kazi ya ujenzi, ambapo eneo linaandaliwa katika uwanja wa Chama cha Mapinduzi, Masiwani.

Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Mohamed Mfundo, ambaye pia ni Diwani wa Kiomoni, imefanya ziara ya kutembelea miradi ikiwa ni maandalizi ya vikao vya kamati vya robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Ziara hiyo ilianzia katika eneo la ufukwe Raskazone maarufu kama Jet ambako kamati ilikwenda kuona mazingira ya eneo hilo la kupumzikia na kupata taarifa za uendelezaji wa eneo hilo ambapo kamati ilitaarifiwa kuwa, tayari michoro iko tayari na fedha kiasi cha shillingi million 20 zimetengwa kwa ujenzi wa kibanda cha huduma na vinywaji katika eneo hilo.

Kamati ilitembelea shule ya msingi Bombo iliyopo kata ya Central kujionea uchakavu wa jengo la awali la shule hiyo linalokisiwa kujengwa mwaka 1902 ambalo kwa sasa halitumiki kutokana na kuwa hatarishi. Jengo hilo la ghorofa moja lililojengwa tangu enzi ya wakoloni, linanyufa kubwa, na maeneo mengine yakiwa tayari yamekatika na kuanguka.

Kamati pia ilitembelea kituo cha afya Mwakidila, katika kata ya Tangasisi, na Geza, kata ya Marungu, kuona eneo lililotengwa kujengwa Zahanati, pamoja na eneo la ujenzi wa soko la Machinga, lililopo kati ya maegesho ya Malori na kituo cha mabasi Kange.

Katika kituo cha afya cha Mwakidila, Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dkt Catherine Rocky ameiambia kamati kuwa kituo kiliingiziwa shillingi million 238 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa jengo la wagonjwa wa ndani (IPD), jengo la Utawala na jengo la huduma ya Mama na Mtoto.

"Katika ajira mpya zilizotoka, kituo chetu kitapata watumishi saba (7), ambapo miongoni mwao kuna madaktari wawili, manesi wawili, ila bado tuna mahitaji wa watumishi, hawatoshi" amesema Dkt. Rocky.

Katika mtaa wa Geza, kamati ilijionea eneo la ekari 3.5 patakapojengwa zahanati ya Geza na tayari kiasi cha shillingi million 225 zimetolewa na Halmashauri kwa kazi hiyo.

Kamati pia ilitembelea eneo la Machinga, ambapo kiasi cha zaidi ya shillingi million 540 kitaanza kazi ya ujenzi wa eneo hilo.

Baada ya kukamilika kwa ziara ya kamati za Mipango Miji siku ya jumatatu, na kamati ya Uchumi siku ya jumanne, siku ya alhamisi itafanyika ziara ya kamati ya kudhibiti UKIMWI na kumalizia na kamati ya fedha siku ya Ijumaa, Julai 29, 2022.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.