• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

WAZAZI NA WALIMU KUSHIRIKIANA KUBORESHA ELIMU

Imewekwa: March 22nd, 2023

Mradi wa uboreshaji mazingira ya utoaji elimu nchini(SHULE BORA) unaotekelezwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Shirika la Misaada la Uingereza (UKaid), umeendesha mafunzo kwa Walimu Wakuu, Wenyeviti wa Kamati za Shule, pamoja na Maafisa Elimu Kata wa Jiji la Tanga kwa lengo la kuwapatia uelewa, mbinu na miongozo ya uanzishaji, utekelezaji na usimamizi wa Ushirikiano wa Wazazi na Walimu (UWAWA) katika elimu ya awali na msingi.


Akifungua mafunzo hayo ya siku tatu, yaliyoanza leo, Jumatatu Machi 13, 2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri,  Afisa Elimu Awali na Msingi wa Jiji la Tanga, Mwl. Kassim Kaoneka amesema lengo la kuunda umoja huo ni kuwaleta pamoja walimu na wazazi katika kusaidiana ili kuhakikisha kunakuwa na mazingira mazuri ya kujifunzia na kufunzia.


"Kufanya vizuri kwa mtoto au kufanya vizuri kitaaluma, kunamtegemea mwanafunzi mwenyewe, Mwalimu, Mzazi au Mlezi, lakini na mazingira yote, hata njia anayoitumia kwenda na kutoka shule. Vyote hivyo vinachangia katika kufanya vizuri kwenye taaluma au kufaulu kwa mtoto" Amesema Kaoneka.


Kaoneka amesema umoja huo wa ushirikiano wa wazazi na walimu utasaidia kuimarisha usimamizi na uendeshaji katika utoaji wa elimu ya awali na msingi kwa kupunguza utoro, mdondoko wa wanafunzi na kuimarisha elimu jumuishi.


"Mtoto anatakiwa awahi shule asubuhi, akichelewa atavikosa vipindi vya mapema, mtoto anatakiwa apate sare za shule, mtoto anatakiwa asiwe mtoro, na ili asiwe mtoro, Mazingira shuleni yanatakiwa kuwa mazuri, ili asiwe mtoro, shuleni kuwe na chakula". Ameeleza Kaoneka.


Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, wameeleza matumaini yao kwa kuanzishwa kwa uWAWA kwamba utaleta ushirikiano mzuri kati ya wazazi na walimu na hivyo kuboresha utendaji na kuinua kiwango cha taaluma.


Mradi wa SHULE BORA ni program mpya ya elimu inayolenga kuinua ubora wa elimu jumuishi inayotolewa kwenye Mazingira salama ya kujifunzia kwa wasichana na wavulana kwenye shule za umma nchini chini ya shirika la Misaada la Uingereza (UKAID) na kutekelezwa katika mikoa tisa ya Tanzania Bara.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.