• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

VIFAA TIBA

Imewekwa: July 7th, 2022

MSTAHIKI MEYA APOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA

Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe. Abdulrahman O. Shiloow amepokea msaada wa vifaa tiba kwa ajili ya maandalizi ya kambi ya Madaktari Bingwa wa magonjwa ya masikio, pua na koo (ENT) vyenye thamani ya zaidi ya shilling millioni 12.5, kutoka Shirika la United Help for Tanzanian Children (UHTC) na United Help for International Children (UHIC)

Hafla fupi ya makabidhiano hayo imefanyika katika Kituo cha Afya cha Mikanjuni, ambapo kwa upande wa UHTC na UHIC waliwakirishwa na Mkurugenzi wa UHTC Dkt. Regis J. Temba na Mwenyekiti Bw. Joseph Desideri Geheri.


Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Diwani wa Kata ya Mabawa Mhe. Athumani I. Babu, Mganga Mkuu wa Jiji Dkt. Charles Mkombe, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mikanjuni Dkt. Ummykulthum A. Kipanga, Wafanyakazi wa kituo cha afya Mikanjuni pamoja na wadau wengine.

Akisoma taarifa ya maandalizi ya kambi hiyo, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mikanjuni Dkt. Ummykulthum A. Kipanga amesema Halmashauri imepanga kufanya kambi ya matibabu kwa kutumia madaktari bingwa wa magonjwa ya masikio, pua na koo (ENT) inayotarajiwa kuanza tarehe 10 hadi 15 mwezi Augosti 2022.

“Kambi hiyo inatarajiwa kuhudumia wagonjwa 300 (screening) ambao kati ya hao takribani wagonjwa 100 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji” amesema Dkt. Kipanga.


Na kwa upande wao, Mkurugenzi wa UHTC Dkt. Temba na Mwenyekiti Bw. Desideri wamesema shirika limekuwa likisaidia dawa kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kwa Vituo vya Afya vya Mikanjuni, Pongwe na Mafuriko zenye thamani ya zaidi ya shilling million mbili kwa kila mwezi lengo likiwa ni kuwezesha watoto kuwa na afya iliyo bora na jamii inayowazunguuka wapate matibabu.

“Na kuhusu kambi kwa ajili ya matibabu ya ENT, UHTC imesaidia vifaa vyote vilivyoombwa kwa kuzingatia vifaa ni muhimu katika utendaji. Na mstahiki Meya tutakabidhi vifaa hivi pamoja na risiti tulizonunulia, na orodha ya vifaa vyote ipo, tutakabidhi” amesema Dkt. Temba.


Akipokea msaada huo, Mstahiki Meya Shiloow amemtaka Mganga Mkuu wa Jiji kuhakikisha vifaa vilivyotolewa vinatumika kama ilivyokusudiwa wakati wa kambi hapo mwezi Augosti.

“Uaminifu ni pamoja na kumfanya mfadhili atimize lengo lake la utoaji wa msaada. Sasa sio leo mkose gloves, muanze kuchomoa kwenye hizi, hapana. Mhifadhi vizuri ili kutimiza lengo la mtoaji wa msaada” amesisitiza Meya Shiloow.

Mheshimiwa Shiloow pia ametumia hafla hiyo kuwaasa watumishi wote wa kada ya afya katika Jiji la Tanga kuimarisha ‘customer care’ (huduma kwa wateja), akiwataka kutumia lugha nzuri akisema haoni sababu za watu kukimbilia huduma katika vituo vya afya vya binafsi wakati vituo vya Serikali (Halmashauri) vina staff (Wafanyakazi) wa kutosha.

Hivyo amewataka watumishi hao wa afya kuwahudumia wagonjwa kwa moyo mkunjufu na iwapo kuna mahali wanakwama, basi watoe taarifa.

Kambi ya mwaka huu inatarajiwa kuwa na madaktari bingwa kutoka Zanzibar.


Labani.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.