• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

UJENZI WA SHULE YA BOMBO WAKAMILIKA

Imewekwa: May 18th, 2018

 Katika kuhakikisha sera ya elimu bure kutoka kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli inatekelezwa, Serikali inatoa zaidi ya milioni 200 kwa kila mwezi katika Jiji la Tanga ili kuboresha elimu. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kwenye uzinduzi wa majengo mapya ya shule ya msingi Bombo iliypo kata ya Central jijini Tanga.

Akizungumza katika ufunguzi huo Mhe. Ummy amesema kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha inatatua changamoto za elimu nchini, ambapo kwa jiji la Tanga katika shule za msingi serikali imetenga milion 50 na sekondari imetenga milion 108.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Bw.Daudi Mayeji amebainisha mikakati iliyofanywa na halmashauri ili kuhakikisha shule hiyo inakuwa ya kisasa na wanafunzi waweze kujisomea katika mandhari nzuri. “Tulichukua  maamuzi ya haraka, kwanza kabisa kusimamisha matumizi na kuwapeleka shule ya jirani, kisha kuanza kufanya ujenzi mpya kwa kiwango bora kama inavyoonekana” alisema Mkurugenzi Mayeji

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Madiwani katika shughuli ya kukabidhi majengo hayo kwa uongozi wa shule hiyo, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mustapha Selebosi ameeleza kuwa halmashauri imechangia zaidi ya milioni 279 kutoka kwenye mapato yake ya ndani. Meya pia, aliendelea kwa kuishukuru serikali kwa kupatia Jiji la Tanga fedha zaidi ya milioni 136 kupitia mradi wa Matokeo Kwanza “Education Programme For Results (EP4R)” ambazo nazo zimewasaidia sana kwenye kuimarisha na kuboresha miundombinu ya shule nyingine jijini humo.

Nao wanafunzi wa shule hiyo walionesha kufurahia kitendo cha kukabidhiwa shule yao. “Tunaishukuru halmashauri kwa kutujengea madarasa mapya, tumefurahi kwani ni madarasa mazuri na sasa tutasoma vizuri zaidi maana kule tulipopelekwa kwa muda tulikuwa tupo wengi darasani lakini sasa tutakaa vizuri na kusoma vizuri pia” walisema baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.

Shule ya msingi Bombo ni miongoni mwa shule tatu za umma zilizopo ndani ya kata ya Central ikiwa na jumla ya wanafunzi 1158 wavulana wakiwa 620 na wasichana 538 huku jumla ya walimu 23 wanaume 3 na wanawake 20.

Shule hii ilijengwa mwaka 1902 na kuanza kutumika kama shule ya awali mwaka 1945 ikimilikiwa na Taibal Sachak kabla ya kutaifishwa na serikali baadae ilianza kutumika kama shule ya msingi hadi mnamo mwaka 2015 ilipositishwa matumizi kutokana na uchakavu hatarishi.


Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.