• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

TANGA YAWAKUMBUKA MASHUJAA

Imewekwa: July 25th, 2022

TANGA YAWAKUMBUKA MASHUJAA

Na: Mussa Labani

Kitengo cha Mawasiliano serikalini Jiji la Tanga.


Mkuu wa Wilaya ya Tanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Mhe. Hashim Mgandilwa leo Jumatatu Julai 25, 2022, amewaongoza wakazi wa Wilaya ya Tanga katika maadhimisho ya siku ya mashujaa iliyofanyika katika bustani ya uhuru (Uhuru Park) katikati ya Jiji la Tanga.


Maadhimisho hayo ambayo yamehudhuriwa na askari wastaafu walioshiriki vita mbalimbali za ukombozi na utunzaji wa amani, ikiwemo vita ya kumaliza uchokozi wa Idd Amin wa Uganda na Tanzania, utunzaji wa amani huko Darfur, na maeneo mengine, yalianza kwa sala na dua kutoka kwa viongozi wa dini.


Katika dua na sala zao, viongozi hao wa kidini, Sheikh wa Mkoa wa Tanga Ally Juma Luwuchu wa Baraza la Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA), MT 30580 SGT Mstaafu Joseph Mhilu wa Kanisa la Anglikana, na Fr. Joseph A. Mbena wa Kanisa Katoliki Tanga, wamewaombea dua na kusihi watanzania kudumisha amani.


Akitoa hutuba fupi katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Mgandilwa amepongeza juhudi kubwa zilizofanywa na wazee waliojitoa kuipigania nchi na kujenga amani ambayo tunapaswa kuilinda na kuienzi.


Mgandilwa amesema tunapaswa kuwa na moyo kama wa wazee wetu, amesema wazee wetu wamefanya wajibu wao kuhakikisha Tanzania inakuwa salama.


"Tunatakiwa tudumishe amani tuliyo nayo kama njia ya kuwaenzi hawa wenzetu. Vinginevyo tutakuwa hatuwatendei haki wenzetu waliotangulia mbele za haki. Nchi yetu ipo salama, ni njema tukabainisha ile mianya yote inayoweza kupelekea uvunjifu wa amani. Tuibaini na tuizuie." Ameasa Mheshimiwa Mgandilwa.


Awali, mwakilishi wa mashujaa Mzee Stephen Ignatius Mponji ameishukuru Serikali kwa kuwakumbuka na kuendelea kuuenzi mchango wao katika ujenzi wa taifa, huku akiwaasa askari walio makambini kuzingatia mazoezi, ukakamavu na nidhamu.


"Sisi tulijitoa mhanga, tuliisaidia nchi yetu kile kipande cha ardhi kilichotekwa pale Kyaka. Niwasisitize wapiganaji mlio kambini, mzingatie mafunzo na nidhamu, nasisitiza ni muhimu sana" amesisitiza Mzee Mponji.


Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe Abdulrahman Shiloow, Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Ndg. Sipora Liana, Katibu Tawala Wilaya ya Tanga, Ndg. Dalmia Mikaya, Viongozi wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Watumishi wa Jiji la Tanga pamoja na wananchi kwa ujumla.


Baada ya maadhimisho hayo, Mkuu wa Wilaya aliwaongoza viongozi kwenda hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga,  Bombo, kumjulia hali Mzee Mbega Salum mkazi wa Magomeni aliyeshiriki vita ya pili ya dunia aliyelazwa katika hospital hiyo, akikadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 95 na 102,  huku Mkurugenzi wa Jiji akiwashika mkono askari mashujaa waliohudhuria shughuli hiyo.



Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.