• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

TANGA JIJI YAANZA UJENZI WA SHULE ZA GHOROFA.

Imewekwa: January 16th, 2025

Januari 9, 2025.


Halmashauri ya Jiji la Tanga imeanza kutekeleza mpango wake wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa majengo ya ghorofa, ambapo kwa mwaka huu wa 2024/2025, shule nne za msingi za Mbuyuni, Majengo, Martin Shamba na Ngamiani Kusini, zimewekwa kwenye mpango wa ujenzi wa majengo hayo, na tayari kazi hiyo ipo kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji.


Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ya Halmashauri ya Jiji la Tanga, leo alhamisi, Januari 9, 2025, ikiwa katika ziara yake ya kawaida ya kila robo mwaka ya kukagua shughuli zinazotekelezwa na Idara na Vitengo vya Halmashauri vinavyo simamiwa na Kamati hiyo, ilitembelea ujenzi wa jengo la madarasa ya ghorofa linalojengwa katika Shule ya Awali na Msingi ya Mbuyuni iliyopo kata ya Nguvumali, ambapo ilipokelewa na uongozi wa Mtaa, Shule na kamati za ujenzi.


Akizungumzia ujenzi huo, Kaimu Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Dorothy Mapunda, amesema ujenzi wa jengo hilo ambalo tayari limeingiziwa shillingi million 350, litakapokamilika, litawapatia wanafunzi na walimu, mazingira mazuri ya kujifunzia na kufunzia, kwani majengo ya awali yalikuwa ni hatarishi kutokana na uchakavu wake.


Jengo hilo litakapo kamilika, litakuwa la ghorofa mbili(sakafu tatu) zenye vyumba 12 vya madarasa( vinne kila sakafu), vyoo na ofisi za walimu. Shule ya msingi Mbuyuni ina jumla ya wanafunzi 402.


Katika ziara hiyo, Kamati iliongozwa na Kaimu Mwenyekiti Mhe. Selebosi Mustafa, ilitembelea na kukagua eneo la ujenzi wa Zahanati ya Msambweni kata ya Msambweni, eneo la dampo Mwang'ombe, kata ya Tangasisi, ambalo Halmashauri inakusudia kupabadilisha matumizi kwa kujengwa viwanja vya michezo vya kisasa.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.