• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

SOKO LA KISASA KUJENGWA MGANDINI

Imewekwa: November 9th, 2023

Na: Mussa Labani, Tanga.

Halmashauri ya Jiji la Tanga inakusudia kutumia kiasi cha zaidi ya shillingi million 18 kukarabati soko la Mgandini ili kuondoa changamoto za miundombinu ya njia, vyoo, ikiwa ni pamoja na maboresho ya vizimba vya nazi, ili kuwawezesha wafanyabiashara wa soko hilo pamoja na wateja kupata huduma katika mazingira yaliyo bora wakati wa majira yote ya mwaka.


Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga, inayofanya ziara ya siku mbili ya ukaguzi wa utekelezaji wa ilani, Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Ndg. Said Majaliwa amesema Halmashauri yake imesikia kilio cha wafanyabiashara hao, ambao aliwatembelea wiki iliyopita na kuagiza wataalam kufanya tathmini ya kuondoa kero hizo, ambapo makisio ya Tsh. 18,192,600.00 yamewasilishwa ili kuondoa changamoto za soko hilo wakati wakisubiri ufadhili wa ujenzi wa soko la kisasa katika eneo hilo.


"Hatuwezi kuwaacha wafanyabiashara wetu hawa wakae na kufanya biashara zao katika mazingira magumu, kwa kusubiri fedha za ufadhili wa ujenzi wa soko. Tutaendelea kuwaboreshea mazingira yao" Amesema Majaliwa.


Mradi wa ujenzi wa soko la kisasa la Mgandini upo kwenye mpango wa kuidhinishwa kwa awamu ya pili ambao unakadiriwa kugharimu kiasi cha zaidi ya shilling billioni 30 katika mradi wa Green and Smart Cities.


Kamati hiyo ya Siasa Mkoa iliyoongozwa na Katibu wa CCM Mkoa, Ndg. Selemani Sankwa, ilitembelea Makazi ya Wazee wasiojiweza Mwanzange yaliyopo Kata ya Duga, ambapo walielezwa kuwa kituo hicho chenye uwezo wa kuhudumia Wazee 34, kwa sasa kina wazee 15 (Kiume 10, kike 5) na kwamba kinakabiliwa na upungufu wa watumishi hasa kada ya upishi, uchakavu wa majengo na mfumo wa umeme.


Katika eneo la Hospitali ya Wilaya, Kamati ilifahamishwa kuwa huduma zote za msingi zinatolewa Hospitalini hapo, ikiwa ni pamoja na huduma za mama na mtoto, picha na mionzi, kinywa na meno, macho na nyinginezo, huku ukarabati wa chumba cha upasuaji uzazi pingamizi (Maternity theater) ukikamilika tayari kwa matumizi.


Hospital ya Jiji la Tanga ilianza kujengwa mwaka 2018 kama Hospital ya Wilaya ambapo kwa awamu ya kwanza yalijengwa majengo saba ambayo ujenzi wake umekamilika na kuanza kutoa huduma mbalimbali, huku awamu ya pili zikijengwa wodi tatu ambazo ziko hatua ya umaliziaji, mradi huo ukitumia zaidi ya shillingi billioni 1.9, Halmashauri ikitegemea kutumia  shillingi million 160 kwa nusu ya mwaka huu wa fedha kukamilisha wodi ya watoto na wanaume.


Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa itaendelea katika siku yake ya pili kwa kutembelea jengo la kitega uchumi Kange na maeneo ya kutolea huduma za afya katika kata ya Pongwe.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.