• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

RAS TANGA APONGEZA VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI KWA UTOAJI WA TAARIFA

Imewekwa: July 12th, 2024

Na: Mussa Labani, Tanga.

Juni 28, 2024.

Katibu Tawala Mkoa wa Tanga (RAS), Ndg. Pili Mnyema, amewataka Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano Serikalini wa Mkoa wa Tanga, kutumia dhamana waliyopewa katika kusimamia Vitengo vya Mawasiliano Serikalini kwa kutoa taarifa sahihi kwa jamii juu ya shughuli za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali, ili kuondoa taarifa za uzushi.


Mnyema amesema, jamii ikipata taarifa sahihi, taarifa za uzushi hazitaweza kusambaa na kuipotosha jamii. Amesema Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeleta fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali ili kutatua kero za wananchi. Amesema ni vizuri jamii ikafahamu kazi kubwa inayofanywa na Serikali yao, na hivyo Maafisa Habari wana wajibu wa kutoa taarifa za utekelezaji wa miradi hiyo.


RAS Mnyema amesema hayo wakati akiwapongeza Wakuu wa Vitengo vya Habari na Mawasiliano Serikalini, katika Mkoa wa Tanga vilivyopata tuzo katika utoaji wa taarifa za kazi za Serikali, ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kufuatia tathmini iliyofanywa na Wizara ya Habari, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa kuangalia namna Wizara, Taasisi, Ofisi za Mikoa na Halmashauri zinavyotoa taarifa kwa umma kwa kipindi cha mwaka 2023/2024.


Akizungumzia umuhimu wa vitendea kazi kwa Vitengo hivyo, Mnyema amesema, kufuatia mabadiliko makubwa katika teknolojia ya habari, ipo haja ya Vitengo kupatiwa vifaa vya kisasa ili watendaji wake waweze kufanya vizuri zaidi.


"Kwa Mkurugenzi hapa (Mkurugenzi wa Jiji la Tanga), sasa ni fursa kwako, kuhakikisha kwamba, tunaimarisha Kitengo chetu cha Mawasiliano kwa kuwapatia vifaa vya kisasa, lakini pia na kuwawezesha masuala ya usafiri kwenda kuzunguuka kwenye miradi, najua Halmashauri ya Jiji tuna miradi mingi sana ambayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuletea fedha za kutosha, kwa hiyo tuna kazi kubwa ya kuhabarisha umma nini kimefanyika katika kipindi cha awamu ya Sita ya Serikali" Amesema RAS Mnyema.


Vitengo vya Mawasiliano Serikalini vilivyopata tuzo ni kutoka Halmashauri ya Jiji la Tanga, ambayo ilishika nafasi ya tisa (9) kati ya 184, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ya tisa (9) kati ya 26 na Tanga UWASA ya sita (6) kati ya 84.


Tathmini hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya kuimarisha mawasiliano ya Serikali kwa umma, lengo likiwa ni kuwafanya Maafisa Habari kutoa taarifa kwa kina kwa wananchi kuhusu miradi yote ya maendeleo.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.