• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

NIPO TAYARI KUANZA KAZI - MGUMBA

Imewekwa: September 9th, 2022

Na.  Mussa Labani. Tanga.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Omary Mgumba amesema yupo tayari kuanza kazi baada ya kuhitimisha ziara ya kujitambulisha kwa Wilaya na Halmashauri za mkoa wa Tanga.


Mgumba ameyasema hayo alhamisi Septemba 8, 2022 wakati akihutubia Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani la Jiji la Tanga uliokuwa na lengo la kujitambulisha kwa Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Jiji, ikiwa ni kituo cha mwisho cha ziara yake.


Akihutubia mkutano huo, Mgumba amelipongeza Jiji la Tanga kwa kufanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato na kuongoza majiji mengine hapa nchini katika mwaka wa fedha 2021/2022 kwa kukusanya mapato kwa asilimia 113 ya lengo la mwaka.


Mgumba amesema dhana ya ugatuaji madaraka inataka Halmashauri kujikusanyia mapato na kutoka kwenye utegemezi wa kusubiri fedha kutoka Serikali Kuu.


Amesema Halmashauri zinapaswa kuondoka kwenye mazoea ya ujenzi wa madarasa, vyoo na vituo vya afya pekee, na kuanza kufikiri kuwa na miradi ya kiuchumi itakayo kuwa chanzo cha mapato  badala ya kusubiri kukusanya ushuru pekee kwa wananchi.


"Mapato ni kipaumbele cha pili baada ya usalama. Na mapato haya yaende kutatua shida za wananchi. Mtu asijaribu kucheza na fedha hizi, Mheshimiwa Rais amekwisha sema, ukitaka kujua rangi yake, basi chezea fedha hizi." Amesema Mgumba.


Mheshimiwa Mgumba ambaye aliongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, aliwataka Madiwani kuhakikisha kunakuwa na msawazo/mtawanyo wa fedha za utekelezaji wa miradi ili kila kata ipate mradi kwa maendeleo ya wananchi, badala ya miradi mingi na mikubwa kuwekwa katika kata moja, huku akishauri utengaji wa fedha uwe wa kutosha kukamilisha mradi ili kuwezesha huduma kutolewa kwa wananchi.


Awali, akiwasilisha taarifa ya Jiji la Tanga kwa Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi wa Jiji Ndg. Sipora Liana amesema kwa mwaka wa fedha 2021/2022 unaoishia mwezi Juni 2022, Halmashauri imefanikiwa kupeleka katika miradi mbalimbali ya maendeleo zaidi ya shillingi billion 6.6 ikiwa ni katika utekelezaji wa utoaji wa asilimia 60 ya mapato ya ndani.


"Kati ya fedha hizi, shillingi 1.1 billion zimeelekezwa katika sekta ya afya, shillingi 2.7 billion sekta ya elimu, shillingi 167 million zimepelekwa eneo la utawala katika ujenzi wa ofisi za kata, na utoaji wa mikopo ya wanawake, vijana na wenye ulemavu ni 1.1 billion, sekta ya biashara ikitengewa million 100 kwa ajili ya ujenzi wa soko, shillingi 410 million zikitumika katika shughuli za anwani za majazi, na miradi mingine ya uwekezaji na ufuatiliaji ikigharimu shillingi 995 million". Amefafanua Liana.


Mkutano huo maalum wa Baraza la Madiwani uliongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe. Abdulrahman Shiloow, ulihudhuriwa na viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.