• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

MWENGE WASIFU MIRADI JIJI LA TANGA, WATOA POLE KWA MAJERUHI WA AJALI

Imewekwa: June 14th, 2023

Juni 10, 2023.


Mwenge wa Uhuru 2023 umemaliza mbio zake katika Wilaya ya Tanga baada ya kukimbizwa umbali wa kilomita 119 kuanzia eneo la mapokezi, Uwanja wa Ndege wa Tanga, hadi kijiji cha Kimang'a Wilayani Pangani ambapo Mwenge huo umekabidhiwa kwa Wilaya ya Pangani.


Akitoa salamu fupi za kuagana katika eneo la makabidhiano, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa kwa Mwaka 2023, Ndugu  Abdallah Shaib Kaimu amesifu utekelezaji na usimamizi mzuri wa miradi iliyopitiwa na Mwenge katika Wilaya ya Tanga.


Ndugu Kaimu amesema Mwenge wa Uhuru 2023 umeridhishwa na ubora wa miradi na uhifadhi wa nyaraka zote muhimu katika utekelezaji wa miradi, ambayo Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ikileta fedha nyingi kuitekeleza, ili kusaidia kuondoa kero kwa wananchi, na hivyo amewataka viongozi wa Wilaya ya Tanga kuendelea kumsaidia Rais kwa kutekeleza miradi hiyo kwa viwango vinavyostahili, huku akisifu ushirikiano mzuri kati ya Chama na Serikali Wilayani Tanga.


Kiongozi huyo pia alitumia muda huo kwa kutoa pole kwa majeruhi wa ajali ya gari iliyokuwa kwenye msafara wa Mbio za Mwenge, na kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awajalie uponyaji wa haraka.

Gari iliyopata ajali ilikuwa moja kati ya gari za matangazo na hamasa, wakati ikitangulia Kijiji cha Kimang'a Wilayani Pangani kwenye eneo la makabidhiano ikiwa na MC, Dj's, Wachekeshaji na Maafisa wengine wa Halmashauri, ilipata ajali umbali mfupi kutoka eneo la Kigombe, ambapo majeruhi walipelekwa Kituo cha Afya Kimang'a kwa huduma ya kwanza na baadae kuhamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga, Bombo.


Awali, akitoa taarifa ya Mbio za Mwenge Wilayani Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Ndg. Hashim Mgandilwa amesema Mwenge umepita katika miradi saba yenye thamani ya shillingi Billion 2.736, ambapo kati ya miradi hiyo, miradi minne imefunguliwa, miwili imetembelewe na mmoja kuwekewa jiwe la msingi.


Akizungumzia mkesha uliofanyika Shule ya Msingi Gofu Juu, Mgandilwa amesema katika mkesha huo, kumefanyika zoezi la utoaji wa chanjo ya Uviko - 19 ambapo watu 102 walichanja, upimaji wa VVU/UKIMWI na uchangiaji wa damu ambapo unit 14 za damu zilipatikana.


Kauli mbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 inasema “Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa Viumbe hai na Uchumi wa Taifa”. Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu ni Mkoani Manyara Oktoba 14, 2023.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.