• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

MISHAHARA KUENDANA NA GHARAMA ZA MAISHA

Imewekwa: April 18th, 2018

Chanzo: HabariLeo (www.habarileo.co.tz)

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeomba kuidhinishiwa bajeti ambayo pamoja na malengo mengine, itaandaa taarifa za gharama za maisha kama msingi wa kukadiria kima cha chini cha mshahara unaoendana na gharama halisi za maisha.

Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali Mitaa katika maoni yake, imeshauri serikali iongeze mshahara kwa watumishi wa umma kuwawezesha kumudu gharama za maisha ambazo zinaongezeka. Akiwasilisha bungeni makadirio ya matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2018/19, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti na Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika ameomba aidhinishiwe jumla ya Sh 669,094,556,009. Kulingana na taarifa ya Waziri, miongoni mwa malengo yaliyopangwa kutekelezwa na ofisi hiyo katika mwaka ujao wa fedha kwa upande wa Bodi ya Mishahara na Masilahi katika Utumishi wa Umma ni kuandaa taarifa nne za gharama za maisha kama msingi wa kukadiria kima cha chini.

“Taarifa hizi zinaweza kushauri kuhusu mshahara wa chini unaoendana na gharama halisi za maisha, “ alisema Mkuchika katika hotuba yake. Chini ya eneo hilo la mishahara na maslahi kwa utumishi wa umma, kupitia bajeti hiyo iliyoombwa, ofisi itafanya utafiti wa hali ya masilahi katika utumishi wa umma nchini na mifumo ya kupima utendaji kazi. Lengo ni kushauri namna bora ya kutoa motisha kwa kuzingatia utendaji ili kuongeza ufaisi katika kuhudumia wananchi. Vile vile itatekeleza mapendekezo yanayotokana na kazi ya tathimini kazi na uhuishaji wa madaraja katika utumishi wa umma.

Ili kutekeleza mpango wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha, Mkuchika alisema Bodi ya Mishahara na Masilahi katika Utumishi wa Umma imeomba kutumia Sh 1,652,435,000 kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Kamati ya Kudumu ya Bunge katika ushauri wake kwa serikali kuongeza mshahara, ilisema wote ni mashahidi kwamba serikali haijaongeza mshahara wa watumishi wa umma kwa mwaka wa tatu sasa.

Ofisi hiyo ya Rais pamoja na mafungu yake imepanga kutekeleza malengo 209, ikiwemo kutoa huduma kwa Rais na familia yake; kumshauri Rais katika maeneo ya uchumi, siasa, masuala ya jamii, sheria, mawasiliano na habari kwa umma, uhusiano wa kikanda, kimataifa na maeneo mengine. Malengo mengine ni kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa mkakati wa taifa dhidi ya rushwa awamu ya tatu (NACSAP III); Kuifanyia mapitio sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya 2007 ili kujumuisha makosa ya uhujumu uchumi na kutaifisha mali zilizopatikana kwa njia ya rushwa na ufisadi.

Imepanga pia kufuatilia matumizi ya fedha za miradi ya maendeleo kwenye taasisi za umma zinazotolewa na serikali na wabia wa maendeleo ili kuhakikisha utekelezaji wake unazingatia thamani halisi ya fedha. Ofisi hiyo ya Rais pia itatumia njia za mawasiliano za kimkakati kufikia kundi la vijana ili washiriki katika shughuli zinazowajengea maadili na hivyo kujenga jamii inayochukia rushwa.

Vile vile itafanya utambuzi na uandikishaji wa kaya masikini zipatazo 355,000 katika vijiji 4,408, mitaa 1,189 na shehia 96 ambazo hazikufikiwa katika awamu ya kwanza. Aidha itaweka na kuhuisha mfumo wa utunzaji wa kumbukumbu za kiutendaji za watumishi katika taasisi za umma 58 ili kuboresha utoaji wa huduma. Hata hivyo kamati katika taarifa yake ilisema uchambuzi wake umebaini kiasi kilichoombwa na ofisi kuidhinishiwa kimepungua kwa Sh 152,227,791,665 sawa na asilimia 18.53 ikilinganishwa na bajeti iliyoidhinishwa katika mwaka wa fedha 2017/18 ambayo ilikuwa Sh 821,322,347,674. Kwa mujibu wa kamati, kiasi kilichopungua ni kikubwa zaidi kwani ni takribani mara tatu ya kiasi kilichopungua katika mwaka wa fedha unaoisha ambacho kilikuwa asilimia 6.89.

Habari hii imetoka kwenye mtandao wa Gazeti la HabariLeo. Bonyeza hapa kuisoma kutokea HabariLeo mtandaoni

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.