• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

MEYA AITAKA HALMASHAURI KUWA NA MPANGO WA UNUNUZI PIKIPIKI ZA WATENDAJI KATA

Imewekwa: February 22nd, 2023

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Mhe. Al-Hajj Abdulrahman Shiloow ameitaka Halmashauri hiyo kuanza utaratibu wa kutenga fedha katika bajeti yake ya mapato ya ndani kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki za Watendaji wa Kata kwa kuanzia na Kata zilizo pembezoni na zenye mazingira magumu ya usafiri.


Al-Hajj Shiloow ameyasema hayo leo, Jumanne, Februari 21, 2023 wakati akikabidhi pikipiki kwa Mtendaji wa Kata ya Pongwe Jijini Tanga Bi. Erica Njama ikiwa ni moja ya pikipiki 916 zilizotolewa na Serikali kupitia Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa lengo la kusaidia usafiri kwa Watendaji wa Kata nchini, na kukabidhiwa kitaifa hivi karibuni na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Isdor Philip Mpango, ambapo Halmashauri ya Jiji la Tanga imepata pikipiki moja.


Shiloow amesema zipo Kata kubwa na zilizo mbali, ambazo nazo zinahitajika kupata pikipiki akitolea mfano wa kata ya Maweni, Mabokweni na Chongoleani, huku kata za Kirare na sasa Pongwe tayari zikiwa zimepata usafiri huo.


"Jiji ni kama tumekumbushwa (kwa Serikali kutoa pikipiki kwa Watendaji wa Kata), uwezo tunao lakini hatuweki kipaumbele cha kununua pikipiki. Uwezo wa kununua pikipiki 2 au 3 kila mwaka tunao. Tuliangalie hili kwa kuweka kwenye bajeti zinazokuja ili kila mwaka tupunguze idadi ya Watendaji wanaohitaji pikipiki" amesisitiza Shiloow.


Kwa upande wake Bi. Erica Njama, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia usafiri Watendaji wa Kata utakao wasaidia katika kutekeleza shughuli za kila siku za kuihudumia jamii.


"Nimekuwa nikipata changamoto za kiutendaji kwa sababu kata ya Pongwe ni kubwa na kuna maeneo kuyafikia ni umbali wa kilomita 25 hadi 30. Wakati mwingine unapigiwa simu kuwa kuna tatizo sehemu, lakini huwezi kufika kwa wakati kwa kukosa usafiri.


Ila kupitia chombo hiki ambacho Mheshimiwa Mama yetu, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametupatia, basi, mimi kama mtumishi wake, nitakwenda kuitumia pikipiki hii kuhakikisha nawafikia na kuwatumikia wakazi wa Pongwe" amesema Njama.


Katika makabidhiano hayo, Mstahiki Shiloow amemkabidhi Bi. Njama pikipiki aina ya Boxer, pamoja na kofia ngumu (Helmet) huku akimtaka kukitunza kifaa hicho na kutumia kwa malengo yaliyokusudiwa.


Tukio hilo lililofanyika katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Tanga lilihudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji Bi. Hawa Msuya, Afisa Utumishi Mkuu wa Jiji Bi. Mwanaidi Nondo, na viongozi wengine. Ambapo pikipiki hizo zinakusudiwa kuwawezesha Maafisa hao kuwafikia wananchi kwa urahisi kwa lengo la kuwahudumia na ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika kata zao.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.