• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

MBUNGE JIMBO LA TANGA MJINI ALETA AFYA CHECK

Imewekwa: August 21st, 2023


Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, ambaye pia ni Waziri wa Afya wa Tanzania, Mhe. Ummy A. Mwalimu, amewakaribisha wakazi wote wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kupata huduma ya upimaji wa afya katika kambi maalum ya upimaji wa afya iliyoandaliwa kwa pamoja na Taasisi ya Afya Check, Ofisi ya Mbunge wa Tanga Mjini na Halmashauri ya Jiji la Tanga, itakayoanza tarehe 21 hadi 25 mwezi huu wa Augosti, 2023, katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Usagara, Jijini Tanga.


Mheshimiwa Waziri Ummy ametoa ukaribisho huo wakati akitangaza rasmi ujio wa kambi hiyo katika Jiji na Mkoa wa Tanga ambapo amesema huduma zitakuwa wazi kwa wakazi wote wa Mkoa wa Tanga na kwamba hakuna malipo ya kiingilio wala kujiandikisha, na kwamba itakuwa ni bure kwa wote.


Mheshimiwa Ummy amesema ni vizuri kuwa na utaratibu wa kupima afya kuliko kusubiri mpaka mtu aumwe ndio anakwenda hospitali, na kwamba yapo magonjwa ambayo yakigundulika mapema, upo uwezekano wa kujinasua kwenye tatizo hilo.


"Na kubwa, unaweza, wala usifanye mambo mengi. Unaweza ukafanya mambo kama matatu tu, tunasema 'know your numbers', jua namba zako.

Namba zako ya kwanza, uzito wako. Namba ya pili kuhusu kisukari. Kwa sababu kisukari ndio kinakuja kupelekea magonjwa kama shinikizo la damu, changamoto za moyo, figo, n.k. Na namba ya tatu ni BP, shinikizo la juu la damu" Amesema Waziri Ummy.


Akizungumzia mambo yatakayofanyiwa upimaji, amesema kwa upande wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza yatakayo fanyiwa upimaji ni pressure (shinikizo la damu), Kisukari, Saratani (aina tatu: mlango wa kizazi, matiti na tezi dume), na macho.

Na kwa magonjwa yanayo ambukiza, ameyataja magonjwa ya UKIMWI, Kifua kikuu na Malaria, na iwapo mtu akigundulika na ugonjwa, atapatiwa dawa.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Afya Check, Dr. Isaac Maro ameshauri jamii kujenga utamaduni wa kupima afya japo mara moja kwa mwaka.

Amesema upimaji wa afya sio jambo la gharama kubwa kulinganisha na matumizi yetu ya kila siku, na kwamba kama vile tunavyofanya service ya magari na baiskeli zetu, ni muhimu pia kuangalia afya zetu na kuzilinda.


Huduma kwa kambi ya upimaji wa afya zitatolewa kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 alasiri kwa siku tano za upimaji.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.