• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

MADIWANI WAMALIZA ZIARA DODOMA, WAJIFUNZA UWEKEZAJI.

Imewekwa: February 13th, 2023

 

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wamerejea Jijini hapa baada ya kuhitimisha ziara yao ya siku nne Jijini Dodoma. Ziara hiyo ilianza kwa wao kuwasili Jijini humo Siku ya Jumatano, Februari 08, 2023.

Wakiwa Jijini Dodoma, walianza ziara yao katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupokelewa na Naibu Meya wa Jiji hilo, Mhe. Jamal Ngalya ambaye ni Diwani wa Kata ya Kizota, na Mkurugenzi wa Jiji, Bw, Joseph Mafuru, na baadhi ya wataalamu wa Halmashauri hiyo.

Baada ya mapokezi hayo, Waheshimiwa Madiwani walipokea taarifa ya utekelezaji wa miradi mikubwa mitano ya kitega uchumi inayotekelezwa kwa fedha za mapato ya ndani, na mradi mkubwa wa barabara ya mzunguuko (ring road) unaotekelezwa na fedha za Serikali Kuu, kutoka kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Bw. Joseph Mafuru, ambapo miradi hiyo, inatarajiwa kuwa vyanzo vya mapato kwa Halmashauri hiyo.

Miradi iliyotembelewa na Waheshimiwa Madiwani katika ziara hii, ilihusisha:

  1. Ujenzi wa Jengo la kitega uchumi katika eneo la Mtumba (Mtumba Complex) ambapo ujenzi huu unafanyika kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza ni ujenzi wa jengo la hotel ya ghorofa 5 na kumbi za mikutano 7, kati ya hizo ukumbi mmoja mkubwa ukiwa na uwezo wa kuchukua watu 1000 kwa wakati mmoja, Gharama za mradi huu zikiwa ni shillingi Billion 59.3.
  2. Ujenzi wa soko la wazi la Machinga (Machinga Complex) mradi umekamilika na umegharimu zaidi ya shillingi Billion 9.5, ambapo fedha za mapato ya ndani zikiwa ni shillingi Billion 6.5 huku zaidi ya Machinga 3,000 wakiingia na kufanya biashara zao kwa uhuru.
  3. Mradi wa stendi kuu ya mabasi kujifunza namna Halmashauri inavyoendesha Jengo la Kitega Uchumi la stendi hiyo. Stend hiyo inapokea wastani wa mabasi 300 hadi 350 kwa siku na hutoa huduma mbalimbali kama ukodishaji wa kumbi, kulaza mabasi, magari binafsi, n.k.
  4. Waheshimiwa Madiwani waliweza kujionea mradi wa Hotel - Dodoma City Hotel, inayomilikiwa na Halmashauri hiyo, yenye vyumba vya kulala 85, ambapo mradi huo umegharimu kiasi cha shillingi Billion 11.9 na tayari imepata mwendeshaji.
  5. Mradi wa Ujenzi wa Shule ya mchepuo wa Kiingereza – Msangalalee English Medium Primary School, iliyoanza mwaka huu, 2023.
  6. Mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya mzunguuko (Ring Road) unaotekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu kwa gharama ya shilling Billion 300.

Siku ya Ijumaa, February 10, 2023, Waheshimiwa Madiwani walihudhuria kikao cha Bunge kwa mwaliko wa Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, na Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu ambapo walipata nafasi ya kujifunza shughuli za uendeshaji wa vikao vya Bunge, na kusikiliza Hotuba ya kuhairisha Bunge iliyosomwa na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.

Baada ya kuhairishwa kwa Bunge, Madiwani wa Jiji la Tanga walipata nafasi ya kusalimiana na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na baadhi ya Mawaziri na Wabunge, na baadae wakiwa na Mhe. Ummy Mwalimu, walifanya vikao vya kimkakati na Mawaziri Mh. Mashimba Ndaki, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, na Mhe. Dkt. Anjelina Mabula, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi.

Katika kipindi chote cha ziara hii, Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini ambaye pia ni Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (Diwani kwa nafasi yake kama Mbunge) aliungana na Madiwani wenzie wa Jiji la Tanga katika muda wote wa ziara ikiwemo kuwezesha itifaki za Bungeni.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.