• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

KAMATI ZA MADIWANI JIJI LA TANGA ZAANZA ZIARA ROBO YA NNE 2021/2022

Imewekwa: July 25th, 2022

KAMATI ZA MADIWANI JIJI TANGA ZAANZA UKAGUZI WA MIRADI.

Na: Mussa Labani

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Jiji la Tanga


Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ya Halmashauri ya Jiji la Tanga, leo Jumatatu Julai 25, 2022 imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi iliyo chini ya Idara zinazosimamiwa na kamati hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya vikao vya kamati vya robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022.


Ziara ya Kamati hiyo imeongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Habib N. Mpa, ambaye ni Diwani wa Kata ya Ngamiani Kati, ambapo kamati ilitembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Maweni, na kisha kamati ilikwenda mtaa wa Kwakaheza A na B kuona maendeleo ya mradi wa kupanga, kupima na kumilikisha (KKK).


Katika eneo la Maweni lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya, kamati iliweza kuona eneo la mita za mraba 5132, ambapo kulingana na sheria, ujenzi wa kituo cha afya unahitaji eneo la kuanzia mita za mraba 5000.


Ziara hiyo ambayo ilimjumuisha Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe. Abdulrahman Shiloow, pamoja na wajumbe wengine wa kamati, na baadhi ya wakuu wa idara za Halmashauri, ilipokea taarifa ya mradi wa KKK kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati iliyoundwa na wananchi kusimamia zoezi hilo, Mhe. Mzamil Shemdoe (Naibu Meya mstaafu na Diwani mstaafu wa kata ya Mabawa), ambaye alisema mtaa wao una jumla ya nyumba 648, ambapo nyumba kamili ni 600 na maboma 48.


Amesema kati ya nyumba 648, waliolipa ili  kufanyiwa upimaji na urasimishaji ni 152 ambapo gharama kwa kila kiwanja ni shilingi 130,000.


"Tunajitahidi na kamati yangu kuhamasisha ili watu walipe. Kamati tunakutana kila wiki na tunagawana nyumba za kufuatilia. Hatutaki Mtaa wetu uwe sababu ya zoezi hili kukwama." Amesema Shemdoe.


Zoezi la KKK katika mtaa huo linafanywa na kampuni ya GeoPlan(EA) LTD na zoezi hili linafanyika katika mitaa kumi ndani ya jiji la Tanga, likitekelezwa kwa fedha za mkopo kutoka Serikali kuu kiasi cha shillingi million 400 ambapo fedha zinazolipwa na wananchi zinarejesha kiasi hicho cha mkopo.


Ziara ya kamati ya Mipango Miji na Mazingira imefungua ziara za kamati zingine za kudumu za Baraza la Madiwani ambapo siku ya Jumanne, Julai 26, 2022, Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu itafanya ziara na kufuatiwa na kamati ya Kudhibiti UKIMWI (CMAC) siku ya alhamisi Julai 28, na Kamati ya Fedha na Uongozi ikiwa ni Ijumaa, Julai 29, 2022.


Ziara hizi zinawapa nafasi Madiwani kuona kwa uhalisia hatua za utekelezaji wa miradi, ubora wa miradi na kujua changamoto za utekelezaji kabla ya kuingia kwenye vikao vya maamuzi katika kuleta ustawi wa jamii ya wakazi wa Jiji la Tanga.


Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.