• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

KAMATI YA UKIMWI YARIDHISHWA UTENDAJI CTC PONGWE.

Imewekwa: January 16th, 2025

Januari 8, 2025.

KAMATI ya kudhibiti UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Tanga (CMAC), leo Jumatano Januari 8, 2025, imefanya ziara ya kukagua shughuli za mapambano dhidi ya UKIMWI katika Jiji la Tanga, ikiwa ni ziara yake ya kawaida inayofanyika kila robo ya mwaka, ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Kamati kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025, kinachotarajiwa kufanyika wiki ijayo.


Katika ziara hiyo, Kamati iliongozwa na Mwenyekiti wake, Naibu Meya wa Jiji, Mhe. Rehema Mhina, ambapo ilianza kwa zoezi la ugawaji wa vishikwambi 312 kwa walimu wa shule za Msingi na Sekondari, zoezi lililofanyika katika ukumbi wa Mikutano Ofisi Kuu ya Jiji, na kisha kutembelea Kituo cha Afya Pongwe kuangalia shughuli za huduma za virusi vya Ukimwi (VVU) na UKIMWI (CTC), na kugawa mipira ya kiume (kondomu) katika maeneo hatarishi katika kata ya Pongwe.


Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mhe. Mhina amemshukuru Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujali afya za wakazi wa Jiji la Tanga, kwa kutoa vishikwambi vyenye mada/masomo maalum kwa wanafunzi juu ya stadi za maisha na afya ya uzazi, kujikinga na virusi vya ukimwi, jinsia na mengine ya kumjenga kijana.


Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha CTC katika  Kituo cha Afya Pongwe, Daktari Ramadhani Juma Kayoga, amesema kitengo hicho kilichoanza huduma mwaka 2009, kwasasa kinahudumia kati ya watu 10 hadi 40 kwa siku, na kinatoa huduma kwa watoto kwa siku za jumamosi.


Akizungumzia mafanikio ya kitengo hicho, Kayoga amesema ni pamoja na Kupunguza idadi ya maambukizi ya VVU, Kupunguza idadi ya maambukizi kutoka kwa mama na mtoto, Kuanzishwa kwa clinic ya watoto siku ya jumamosi na Kutoa nauli na kifungua kinywa kwa watoto ili kuwezesha nauli ya kuudhuria clinic.


Kamati imepongeza uongozi wa kituo na wadau wanaoshirikiana nao, Shirika lisilo la Kiserikali la Tanzania Health Promotion Support (THPS), katika jitihada zao za kuelekea zero tatu za hakuna maambukizi mapya, kifo wala unyanyapaa.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.