• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

KAMATI YA FEDHA YAKAGUA MIRADI YA TASAF

Imewekwa: May 29th, 2023

Na. Mussa Labani, Tanga 

Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Jiji la Tanga, chini ya Mwenyekiti wake, Mstahiki Meya wa Jiji, Mhe. Al-Hajj Abdulrahman Shiloow, leo, Ijumaa Mei 26, 2023, imefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa baadhi ya miradi ya ajira za muda inayotekelezwa chini ya mpango wa kunusuru kaya za walengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, TASAF.


Katika ziara hiyo, Kamati imetembelea mradi wa ujenzi wa kivuko cha miguu kilichopo Mtaa wa Mwahako barabarani, Kata ya Masiwani, Ujenzi wa kisima kifupi cha maji, kilichopo Mtaa wa Mapinduzi, Kata ya Duga, mradi wa usafishaji mfereji wa maji ya mvua, uliopo Mtaa wa Swahili Kata ya Magaoni, na upandaji wa miti ya  kupendezesha mji pembeni ya barabara ya Jamathcan kuanzia shule ya Msingi Usagara, Kata ya Usagara.


Akizungumzia manufaa ya mradi wa ujenzi wa kisima kifupi cha maji katika Mtaa wa Mapinduzi kilicho gharimu kiasi cha shilling 820,000, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Athumani Mohamed Mganga, ameiambia Kamati ya Fedha kuwa wameupokea kwa furaha mradi huo kwani kisima hicho kimewawezesha kuwa na uhakika wa upatikanaji wa maji kwa muda wote, tofauti na maji ya bomba ambayo kuna wakati hayatoki.


Mganga ameomba kuangaliwa uwezekano wa kupatiwa pump ili kuondoa adha ya kutumbukia kwa vichota maji, na kwamba maji hayo ni tegemeo kwa wakazi wengi wa mtaani kwake kwa matumizi ya nyumbani, ikiwa ni pamoja na kufua, huku akisifu uzuri wa maji hayo.


"Ila kuna changamoto kubwa ya watoto, watoto wadogo. Tumekubaliana kwenye vikao, kuwa mtoto chini ya umri wa miaka 14 asiruhusiwe kuteka maji ili kuepusha kutumbukia kisimani." amesema Mwenyekiti Mganga.


Kwa upande wake Mratibu wa TASAF Jiji la Tanga Bw. Juma Mkombozi, amesema miradi iliyotekelezwa ilikuwa ni miradi midogo ambayo haikuhusisha uwekaji wa pump kwenye visima vya maji, hata hivyo amesema kipindi cha pili cha utekelezaji kitaanza hivi karibuni na kushauri iwapo jamii husika haitakuwa na hitaji jingine, wanaweza kutumia fedha za kipindi hicho kwa kuweka pump katika kisima chao, baada ya kupata ushauri wa kitaalam.


Awali, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Abdulrahman Shiloow, aliwataka wakazi wa eneo hilo kutoa mrejesho wa ubunifu unaofanywa na Serikali ambao una lengo la kutatua changamoto za wananchi na kurahisisha maisha yao.


Shiloow amesema pamoja na nafasi zao za kuwawakilisha wananchi, lakini pia wanasimamia shughuli za Serikali, hivyo wananchi wanapotoa mrejesho wa utekelezaji wa shughuli za Serikali kunawawezesha kujua mafanikio ya ubunifu huo.


Utekelezaji wa mradi wa ajira za muda katika Mpango wa kunusuru kaya za walengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, utasaidia kuinua uchumi wa kaya kwa kushiriki katika kazi za jamii na kupata kipato cha ziada kwa matumizi ya kaya, na wakati huo wakiboresha miundombinu katika jamii huku wakipata ujuzi na stadi za maisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 17, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI KUJADILI HESABU ZA MWAKA August 29, 2023
  • MWENGE WA UHURU TANGA JIJI May 29, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI KUJADILI HESABU ZA MWAKA August 29, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YARIDHISHWA NA HALI YA LISHE JIJI LA TANGA

    August 21, 2023
  • MBUNGE JIMBO LA TANGA MJINI ALETA AFYA CHECK

    August 21, 2023
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI YA ELIMU, AFYA.

    July 26, 2023
  • KAMATI YA MIPANGO MIJI NA MAZINGIRA YAFANYA UKAGUZI

    July 26, 2023
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.