• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

JIJI LA TANGA LAPONGEZA UWEKEZAJI DODOMA JIJI

Imewekwa: February 10th, 2023

Mussa Labani.

Dodoma, February 9, 2023.

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wameanza ziara yao ya mafunzo katika Jiji la Dodoma kwa kutembelea miradi minne ya kiuchumi inayotekelezwa kwa fedha za mapato ya ndani, ambayo inatarajiwa kuwa vyanzo vya uhakika vya mapato kwa Halmashauri hiyo.


Mara baada ya kufika katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma, msafara huo wa madiwani wa Jiji la Tanga unaoongozwa na Mstahiki Meya Mhe. Al-Hajj Abdulrahman Shiloow, ulipokelewa na Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe. Jamal Ngalya na Mkurugenzi wa Jiji hilo Bw. Joseph Mafuru, ambapo waliweza kupata taarifa za utekelezaji wa miradi na matarajio ya Halmashauri hiyo kwa miradi hiyo.


Akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mkurugenzi wa Jiji Bw. Joseph Mafuru amesema Halmashauri hiyo inatekeleza miradi mingi mikubwa kwa fedha za ndani kwa kujinyima, na kuwekeza katika ujenzi wa miradi ya kiuchumi ili katika siku za usoni, Halmashauri isitegemee kuendesha shughuli zake kwa ushuru wa kukimbizana na wachuuzi wadogo, bali iwe na uhakika wa kupata mapato kutoka katika vitega uchumi vyake.


Mafuru amesema Halmashauri hiyo inajenga jengo la kitega uchumi katika eneo la Mtumba (Mtumba Complex) kwa awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza wanajenga jengo la hotel ya ghorofa 5 na kumbi za mikutano 7, kati ya hizo ukumbi mmoja mkubwa ukiwa na uwezo wa kuchukua watu 1000 kwa wakati mmoja, kwa gharama za mradi zikiwa ni shillingi Billion 59.3.


Halmashauri hiyo pia imetekeleza mradi wa ujenzi wa soko la wazi la Machinga (Machinga Complex) mradi uliogharimu zaidi ya shillingi Billion 9.5, ambapo fedha za mapato ya ndani zikiwa ni shillingi Billion 6.5 huku zaidi ya Machinga 3,000 wakiingia na kufanya biashara zao kwa uhuru.


"Kuna faida nyingi zimepatikaa kwa ujenzi wa lile soko. Kwanza kwa sasa hata mvua zinyeshe, jua haviwapati. Wapo kivulini. Jiji sasa ni safi, sasa hivi unaweza kuiona barabara hadi mwisho, palikuwa pachafu.

Pale kwa sasa hawalipi, lakini tumewapa muda, muda ukiisha wataingia mikataba ambayo watalipa na tunatarajia kukusanya shillingi Billion 1.5 kwa mwaka.


Lakini pia kuna fursa zingine zimejitokeza. Kama kuna maombi ya kuweka mbao kubwa za matangazo(Billboards), kwenda kufanya matamasha, vibanda vya ATM, ambao pia wanalipia" amesema Bwana Mafuru.


Katika ziara hii, madiwani wameweza kutembelea jengo la kitega uchumi la Mtumba, stendi kuu ya mabasi - nanenane, mradi wa Machinga Complex na mradi wa Hotel ya Dodoma Jiji(Dodoma City Hotel) ambapo katika miradi yote hiyo, wamepongeza Jiji la Dodoma kwa uwekezaji mkubwa walioufanya.


Katika stendi kuu ya mabasi, Meneja wa stendi hiyo Bw. Mabrouk Seif alisema stend hiyo hupokea wastani wa mabasi 300 hadi 350 kwa siku na zipo huduma mbalimbali ambazo hutolewa na kituo hicho ikiwemo kumbi, kulaza mabasi na magari binafsi.


Waheshimiwa Madiwani waliweza kujionea mradi wa hotel ya Dodoma City Hotel yenye vyumba vya kulala 85, ambapo mradi huo umegharimu kiasi cha shillingi Billion 11.9 na tayari imepata mwendeshaji.


Jioni ya siku ilikamilika kwa Waheshimiwa Madiwani kukutana na Mbunge wa Jiji la Tanga na ambaye pia ni Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu kwa kikao cha kusalimiana na kubadilishana mawazo.

Na siku ya ijumaa asubuhi Waheshimiwa Madiwani watahudhuria kikao cha Bunge.


Wilaya ya Dodoma ilianzishwa mwaka 1973, mwaka 1980 ilipewa hadhi ya kuwa Manispaa na tarehe 26 April 2018 ilipewa hadhi ya kuwa Jiji.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.