• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

HALMASHAURI YAJITOA SAKATA LA UMILIKI UWANJA WA MZALENDO

Imewekwa: February 3rd, 2023

Mussa Labani, Tanga.

Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Tanga wa robo ya pili kwa Mwaka wa fedha 2022/2023 uliofanyika Jumatano, Februari 01, 2023, umepokea na kuridhia taarifa ya Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Al-Hajj Abdulrahman Shiloow juu ya uamuzi wa Halmashauri kujitoa katika Sakata la uhalali wa umiliki wa eneo la Uwanja wa Mzalendo, uliopo Kata ya Mwanzange karibu na Soko la Mgandini.

Akisoma taarifa ya Mstahiki Meya kwa Baraza, Al-Hajj Shiloow amesema Baraza la Madiwani halina maslahi yoyote na uwanja wa Mzalendo ambao katika mipango kabambe ya Halmashauri ya tangu mwaka 1963 ulidhamiriwa na kupangwa kuwa eneo la makaburi.

Aidha amesema kuwa, Mamlaka ya ubadilishaji wa michoro, matumizi ya ardhi kwa sasa Baraza pamoja na kamati zake halihusiki na halina mamlaka hayo.

Eneo hilo la uwanja wa Mzalendo kwasasa lipo chini ya Taasisi moja ya kidini kufuatia taratibu za kisheria kuonyesha wanahaki ya kumiliki.

Akizungumzia taswira ya Jiji, Mhe. Shiloow ametoa miezi mitatu (03) kwa wamiliki wa majengo mabovu, machafu au yaliyochoka yaliyo katikati ya Jiji kuyafanyia uwekezaji, kuyauza au kuyarekebisha ili yaendane na hadhi ya Jiji la Tanga.

Mstahiki Shiloow ametumia pia mkutano huo kuwataka wasafirishaji wote kuanza na kumalizia safari zao kwa kupita katika stendi ya Jiji iliyopo Kange, na kwa wale wenye terminal (vituo vyao) ambao wamekidhi vigezo, wakitakiwa kupita Kange Stendi dakika 15 kabla ya muda wa kuanza safari na wakilazimika kupita wakirudi safari.

Mkutano huo wa kawaida wa Baraza la Madiwani ulianza kwa kuapishwa kwa Diwani mpya wa Kata ya Mnyanjani Mhe. Simba M. Kayaga wa Chama Cha Mapinduzi ambaye alichaguliwa katika uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni kujaza nafasi ya Marehemu Yakub Nuru Othman aliyefariki Mei 15, 2022.

Awali, Meya Shiloow alimpongeza Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Dkt. Sipora J. Liana kwa kuiongoza Menejimenti ya Halmashauri katika ukusanyaji wa mapato, na hivyo Halmashauri kufanikiwa kuvuka lengo la makusanyo ya mapato kwa nusu mwaka (Julai – Desemba) kwa kuweza kufikia asilimia 50.4, na hivyo kuongoza kimkoa kwa makusanyo.

Matangazo

  • MUDA WA NYONGEZA KULIPA KODI YA PANGO LA ARDHI BILA RIBA February 16, 2023
  • UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI KWA DARASA LA AWALI NA LA KWANZA 2023 December 09, 2022
  • MSAMAHA WA RIBA KWA KODI YA PANGO September 28, 2022
  • MKUTANO MAALUM WA BARAZA LA MADIWANI September 28, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • AKIDAYA WANUFAIKA NA MIKOPO YA HALMASHAURI

    March 22, 2023
  • WAZAZI NA WALIMU KUSHIRIKIANA KUBORESHA ELIMU

    March 22, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI JIJI LAPOKEA RASIMU YA BAJETI 2023/2024

    March 02, 2023
  • KAMATI YA USHAURI WILAYA YAJADILI BAJETI YA BILLION 72.1

    March 02, 2023
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.