• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

HALMASHAURI KUWEZESHA WANAWAKE, VIJANA

Imewekwa: May 7th, 2018

Halmashauri ya Jiji la Tanga, limekusidia kuwezesha vikundi vya wanawake na vijana, hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Bw. Daud Mayeji akiwa kwenye Baraza Maalum la Madiwani lilifanyika kwenye ukumbi wa Jiji la Tanga. “Suala la kuwawezesha wanawake na vijana lipo kisheria na limesemwa kwenye miongozo yetu ya bajeti, sisi kama halmashauri hatuna budi kutekeleza hilo”

Kama ilivyoelekezwa kwenye miongozo, halmashauri ilishawapatia fedha za mikopo baadhi ya vikundi. Pamoja na kutoa fedha hizo, lakini kumekuwa na changamoto nyingi sana kwenye kufanya marejesho ya mikopo hiyo. “Kwa sasa halmashauri inapitia vikundi vyote vilivyopewa mikopo na kuendelea kufanya ufuatiliaji wa marejesho ili fedha hiyo iendelee kukopesha wengine”alisema Mkurugenzi.

Halmashauri inaendelea na taratibu za kutambua vikundi na kuvisajili halmashauri ambapo awali vikundi vingi vilikuwa vimejisali kwa Wakala wa Usajili wa Leseni na Biashara (BRELA). Kitendo hiki ni kinyume na utaratibu wa usajali wa vikundi vilivyokusudiwa kupata fedha hizi. Muongozo wa kukopesha fedha hizi kwa kikundi unataka kikundi lazima kimesajiliwa kwenye halmashauri husika ndipo kipate mkopo.

Nae Afisa Maendeleo ya Jamii, Bi Flora Shija amesema halmashauri inaendelea kutoa elimu ya namna ya kufanya usajili wa vikundi kwenye ngazi ya halmashauri na kuwapa namna bora ya kutumia mikopo hiyo ili kuleta tija ya maendeleo na kuweza kurejesha mikopo. “Hadi sasa tunaendelea kutoa elimu kwa vikundi vya wanawake, vijana, walemavu na wengineo, na tarehe 9 mwezi huu tutakuwa na mafunzo ya usajili wa vikundi vya kiuchumi wa kijamii kwenye ukumbi wa Tangamano hapa jijini Tanga” alisema afisa huyo alipokuwa naongea na mwandishi wa habari hii.

Kwa upande wao, waheshimiwa madiwani wa jiji hilo wameonesha kufurahia mpango wa vikundi kupewa vifaa na vitendea kazi badala ya kupewa fedha maana kumekuwa na mtindo wa wanakikundi kugawana fedha na kushindwa kufanya shughuli kama kikundi, hali hii inapelekea kushindwa kufanya marejesho kama utaratibu wa mikopo unavyotaka.

Kwa mujibu wa sheria na miongozo ya bajeti, Halmashauri zinatakiwa kutoa asilimia 10 ya bajeti ya mapato yake ya ndani 5% kwa wanawake na 5% kwa vijana (vijana wa kike na wa kiume wa miaka kati ya 15 na 35) kiwango hiki hutolewa kama mkopo wenye masharti nafuu kwa makundi hayo ili kuweza kufanya shughuli za kimaendeleo na kisha kurejesha mkopo huo kwa faida ya asilimia 10 kwa mwaka. Kwa mwaka wa fedha 2017/18, halmashauri ya Jiji la tanga limetenga jumla ya Tsh. Milioni 640 kwa ajili ya vijana na wanawake.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.