• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

FAHAMU BOMBA LA MAFUTA KUTOKA HOIMA HADI BANDARI YA TANGA

Imewekwa: August 9th, 2017

UFAHAMU MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI KUTOKA HOIMA NCHINI UGANDA HADI BANDARI YA TANGA-TANZANIA

Mradi huu wa Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga Tanzania Unajulikana kama East African Crude oil Pipeline (EACOP).

Bomba hili litakuwa na urefu wa kilometa 1,445.

Mradi wa Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi kupitia Tanzania ulitangazwa na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati wa Mkutano wa 13 wa ushoroba wa kaskazini ambapo alieleza kuwa Bomba hilo la Mafuta kutoka Hoima Ziwa Albert nchini Uganda litapita katika ardhi ya Tanzani kwenda bandari ya Tanga.

Aidha baadhi ya sababu zilizochangia bomba hilo kupita nchini ni pamoja na:

 i.  Ubora wa bandari ya Tanga ambayo imeonekana kuwa bora zaidi ukilinganisha na bandari nyingine Africa Mashariki kwa kuwa ina kingo za asili (naturally sheltered) na kina cha futi 25 kwenda chini hivyo kupunguza muda na gharama za ujenzi kwa kuwa uchimbaji wa kina hauhitajiki.Aidha bandari hiyo itakuwa na uwezo wa kupakia mafuta katika mwaka mzima.

ii.  Miunganiko ya njia za reli ya Tanga hadi reli ya kati

iii. Miundombinu ya barabara nyingi ambayo haipo katika njia mbadala za jirani.

iv. Usalama na uzoefu wa Tanzania katika ujenzi wa mabomba yakiwemo Bomba la gesi Asilia kutoka kisiwa cha Songo Songo mpaka Ubungo-Dar, Bomba la gesi asiliakutoka Madimba Mtwara hadi Kinyerezi Dar-es-salaam na Bomba la kusafirisha mafuta kutoka Tanzania hadi Zambia (TAZAMA).

v. Hali ya tambarare katika ardhi ya Tanzania hivyo gharama za utekelezaji kuwa rahisi.

TAMKO LA PAMOJA.

Tamko la Pamoja la kukamilika kwa majadiliano ya vipengele vya mkataba kuhusu utekelezaji wa Mradi husika lilisainiwa tarehe 21 Mei,2017 Jijini Dae-es-Salaam na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mhe Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri wa Uganda Mhe.Yoweri Kaguta Museveni

KUSAINI MKATABA.

Waziri wa katiba na Shria wa Tanzania Prof. Paramagamba Kabudi pamoja na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Mhandisi Irene Muloni tar 26/05/2017 walisaini mkataba wa INTERGOVERMENTAL AGREEMENT (IGA)-Yaani mkataba wa ushirikiano kati ya Serikaliya Uganda na Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa Ujenzi wa Bomba la kusafirisha

mafuta ghafi (crude oil) kutoka Hoima nchini Uganda  hadi Bandari ya Tanga Tanzania.

UTEKELEZAJI

Mradi huo mkubwa utatekelezwa kwa ushirikiano wa Serikali za Uganda na Tanzania na pia utahusisha kampuni za TOTAL E & P ya Ufaransa, TULLOW OIL ya Uingereza na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) ya China.Makisio ni uwepo wa mapipa Bilioni 1.2 - 1.7 (recoverable).

GHARAMA

Ujenzi wa Bomba hili la mafuta utagharimu jumla ya Dola za Marekani Bilion 3.55 nalitakuwa na urefu wa kilometa 1,445 ambapo litasafirisha mapipa (200,000) na 216,000 kwa siku. kati ya kilometa hizo kilometa 1,149 zitajengwa ndani ya ardhi ya Tanzania.

FAIDA ZA MRADI

i. Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kuzalisha ajira zaidi ya 11,000 za muda mfupi na za kudumu

ii. Kuchochoa utafutaji wa mafuta nchini Tanzania na nchi Jirani hususan katika maeneo linapopita bomba la mafuta.

iii. Kuimarisha matumizi ya Bandari ya Tanga na hivyo kuongeza mapato ya serikali.

NJIA YA BOMBA LA MAFUTA.

Bomba hili litaingia mkoa wa Kagera kutoka Nchini Uganda na kupitia katika mikoa ya Geita,Shinyanga,Tabora ,Singida,Dodoma na Manyara hadi Bandari ya Tanga.

WATUMIAJI WENGINE WA BOMBA

Nchi zinazotarajia kutumia bomba hilo kwa miaka ijayo ni pamoja na Jamhuri ya  Kidemokrasia ya Congo,Sudan Kusini,Burundi na pia nchi nyingine za Afrika mashariki.

ENEO ITAKAPOJENGWA GATI

Gati itajengwa nje kidogo ya Mji wa Tanga katika eneo la Chongoleani.

SHUGHULI ZA UTAFITI.

Zoezi la utafiti wa nchi kavu na baharini limefanywa.Tayari sampuli za udongo na maji zimekwishapatikana kwa ajili ya uchunguzi wa takwimu mbalimbali za kihandisi. Maeneo 6 yamekwishachimbwa visima vya sampuli za udongo katika awamu ya kwanza.

Utafiti wa njia nzima ya Bomba unaendelea kwa kuanza kuwashirikisha wadau wote wa Mikoa ambayo bomba litapita.

 

MIKOA NA WILAYA AMBAYO BOMBA LITAPITA.

MKOA
WILAYA
KAGERA
Missenyi
Bukoba Rural
Muleba
Biharamulo
GEITA
Geita
Chato
Bukombe
Mbogwe
SHINYANGA
Kahama Town
TABORA
Nzega
Igunga
SINGIDA
Iramba
Mkalama
Singida Rural
MANYARA
Kiteto
Hanang
DODOMA
Kondoa
Chemba
TANGA
Kilindi
Handeni Town
Korogwe Rural
Muheza
Tanga City

Bomba hili linatarajia kukamilika mwaka 2020. Lakini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli amesisitiza mradi huwo kuweza kuisha hata kabla ya mwaka 2020 kwa kushauri wakandarasi wataojenga Bomba Hilo kufanya kazi mchana na usiku ili kukamilisha mradi huo kwa haraka.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.