• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

BUSTANI YA JAMHURI KUJENGWA UPYA

Imewekwa: July 23rd, 2022

BUSTANI YA JAMHURI KUJENGWA UPYA.


Mkataba wa kazi ya ujenzi wa bustani ya kupumzikia ya Jamhuri (Jamhuri Park) maarufu kama Forodhani iliyo kando ya bahari ya Hindi pembeni ya maktaba ya Mkoa wa Tanga, umewekwa saini na tayari mkandarasi amekabidhiwa eneo kwa kuanza kazi za ujenzi wa bustani hiyo.


Ujenzi wa bustani hiyo ni moja wa miradi mikubwa inayotekelezwa katika Jiji la Tanga kwa ufadhili wa Taasisi ya Botnar Fondation kupitia mradi wa Tanga Yetu, na unatarajiwa kugharimu kiasi cha karibu shillingi Billion mbili za Kitanzania.


Lengo la mradi huo ikiwa ni kuboresha sehemu za mapumziko kwa familia, na ambapo vijana wataweza kupata fursa ya kufanya biashara zitakazo waongezea kipato na hivyo kujikimu kimaisha.


Ujumbe wa wasimamizi wa mradi huo ESRF (Economic and Social Research Foundation), Ijumaa Julai 22, 2022 uliwaongoza wakandarasi wa mradi huo kampuni ya V. J. Mistry & Co. LTD ambao ndio walioshinda zabuni ya ujenzi, pamoja na Mhandisi Mshauri wa mradi kuwatambulisha kwa Mkurugenzi wa Jiji na Mstahiki Meya wa Jiji.


Akiongea na ugeni huo Ofisini kwake, Mkurugenzi wa Jiji Ndg Sipora Liana, amemtaka Mkandarasi V. J. Mistry kuhakikisha anaanza kazi mara moja na kukamilisha kazi kwa wakati.


"Hii kazi tumeisubiri kwa muda mrefu sana. Hivyo muanze kazi mara moja na mkamilishe kwa wakati. Tena ujenge hivi hivi kama inavyoonekana kwenye mchoro" alisisitiza Mkurugenzi Liana.


Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji, Mhe. Abdulrahman Shiloow amewataka wakandarasi kuwatumia vijana wa Tanga katika kazi ambazo hazihitaji utaalamu maalum.


"Katika zile nafasi za kazi ambazo sio "professional" hatutarajii kuona unaleta watu kutoka Dar es Salaam wakati hapa Tanga tuna vijana wengi tu. Kwa zile za kitaalamu, sawa. Lakini hizi zingine, vijana wa hapa Tanga wapate nafasi. Na pia nikukumbushe suala la kutoa CSR, unarudisha kwa jamii kile ulichopata, kwa kiwango kilicho ndani ya uwezo wako" amesisitiza Meya Shiloow.


Mradi wa ujenzi wa uboreshaji wa bustani ya Jamhuri(Forodhani) unatarajiwa kuanza hivi karibuni baada ya kupatikana kwa mkandarasi, na shughuli za ujenzi zitakapoanza eneo litafungwa kulingana na mpango kazi wa mkandarasi.


Kukamilika kwa ujenzi wa bustani hiyo kutabadili kwa kiasi kikubwa muonekano wa eneo hilo la Jiji na kufanya mji kupendeza zaidi.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.