• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

BARAZA LA MADIWANI JIJI LAPOKEA RASIMU YA BAJETI 2023/2024

Imewekwa: March 2nd, 2023

Na; Mussa Labani

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Jiji la Tanga limepokea taarifa ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Tanga kwa mwaka 2023/2024 iliyowasilishwa leo, alhamisi Machi 2, 2023 katika mkutano maalum wa Bajeti ulioanza leo na kutarajiwa kuisha hapo kesho.


Akiwasilisha taarifa hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Afisa Bajeti kutoka Idara ya Mipango, Mchumi Maria Ndohelo amesema maandalizi ya Bajeti hiyo yamefuata utaratibu wa maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali (Budget Cycle), sera na miongozo ya Kitaifa na ya Kisekta pamoja na mipango na mikakati mbalimbali, ikiwemo ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala ya Mwaka 2020 - 2025.


Mkutano huo wa Baraza ulioongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe. Al-Hajj Abdulrahman Shiloow, na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Tanga Meja (Mst) Hamisi Mkoba, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Hashim Mgandilwa, Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Dkt. Sipora Liana, ulipitia taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2021/2022, na nusu mwaka ya utekelezaji kwa mwaka 2022/2023.


Katika taarifa za mapitio, wajumbe walieleza kuridhishwa kwao na utekelezaji wa shughuli za Halmashauri, hasa katika eneo la ukusanyaji wa mapato ambapo katika mwaka 2021/2022, Halmashauri iliweza kuvuka lengo la makusanyo kwa kukusanya kwa asilimia 113 ya lengo la makusanyo ya mapato ya ndani, na katika kipindi cha nusu mwaka 2022/2023 kilichoanzia Julai hadi Desemba 2022, Halmashauri pia imeweza kuvuka lengo la makusanyo kwa kukusanya kwa asilimia 50.04.


Katika kipindi hicho pia, Halmashauri imeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kutoka katika fedha za ndani, fedha za Serikali kuu, wafadhili na vyanzo vingine, ikiwemo miradi ya ujenzi wa vituo vya huduma ya afya, madarasa, matundu ya vyoo katika shule, jengo la kitega uchumi, utoaji wa mikopo, n.k.


Akitoa nasaha zake katika Baraza hilo, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mhe Hashim Mgandilwa, ameshauri Halmashauri kufikiria kuanza miradi mikubwa ya uwekezaji itakayokuwa chanzo cha uhakika cha fedha, akitolea mfano wa ujenzi wa Hotel na kumbi za mikutano, ambazo zinaweza kuwekezwa hata nje ya mipaka ya Jiji au nje ya Mkoa wa Tanga.


Mgandilwa pia ameshauri Jiji kuweka utaratibu wa kuandaa maandiko ya kitaalamu kwa ajili ya kuomba fedha za kuanzisha miradi ya uwekezaji badala ya kusubiri za kuletewa.


Katika siku yake ya pili ya mkutano, Baraza litapokea na kujadili mapendekezo ya Mpango na Bajeti kwa mwaka 2023/2024 ambapo makisio ya kukusanya na kutumia jumla ya shillingi 72,111,627,000.00 (Billion 72.1) kwa ajili ya mishahara na matumizi mengineyo, yatawasilishwa.


Mkutano huu ni muendelezo wa vikao vya maandalizi ya Bajeti ya Halmashauri ambapo tayari umetanguliwa na vikao vya Menejimenti, wadau, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC), Baraza la Wafanyakazi, na Kamati za Kudumu za Halmashauri, ambapo kesho ijumaa Machi 3, 2023 vinahitimishwa katika siku ya pili ya Mkutano wa Baraza la Madiwani tayari kwenda ngazi ya Mkoa, Wizara na hatimaye Bungeni.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.