• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

ANDIKISHENI WATOTO SHULE KABLA YA JANUARI 2023

Imewekwa: December 23rd, 2022

Na; Mussa Labani, Tanga.

Wito umetolewa kwa Wazazi na Walezi katika Jiji la Tanga, wenye watoto waliofikia umri wa kuanza shule katika madarasa ya awali na darasa la kwanza, kuwaandikisha kabla au ifikapo Desemba 30, 2022, tarehe iliyopangwa kama muda wa ukomo wa uandikishaji watoto kwa mwaka wa masomo unaoanza Januari 2023.


Wito huo umetolewa alhamisi, Desemba 22, 2022, na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Al-Hajj Abdulrahman Shiloow wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya hali ya uandikishaji wa wanafunzi kwa madarasa hayo.


Al-Hajj Shiloow amesema, tofauti na ilivyozoeleka kwa miaka mingi iliyopita kuwa, uandikishaji huendelea kwa miezi hadi mitatu tangu shule kufunguli, lakini kwa wakati huu, Serikali imepanga zoezi hilo kufungwa mwisho wa mwezi huu wa Desemba, hii ni kuwezesha watoto wote kuanza masomo kwa pamoja kuondoa muachano wa ufundishaji.


"Naomba nichukue fursa hii, kuwaomba na kuwasihi, wazazi na walezi katika Jiji hili la Tanga, na maeneo mengine yote ya Tanga, kwamba uandikishaji wa watoto katika madarasa yetu ya awali na la kwanza, utamalizika tarehe 30 Desemba.


Niwaombe shime wazazi wote, wenye watoto wa kike na kiume, wenye ulemavu na wasio na ulemavu, mwisho ni tarehe 30 mwezi huu, shule zipo wazi, walimu wapo kwa ajili ya shughuli za shule, uandikishaji unaendelea katika shule zote 81 za Halmashauri, uandikishaji ni bure, hakuna kitu chochote utakacho chajiwa." Amesisitiza Mstahiki Meya Shiloow.


Umri wa kuandikishwa kwa wanafunzi wa darasa la awali ni miaka 4, wakati wale wa darasa la kwanza ni miaka 6.

Kwa mujibu wa takwimu zilivyo sasa, wanafunzi walioandikishwa kwa darasa la awali katika shule za Serikali kwa Jiji la Tanga ni 3,122 kati ya matarajio ya kuandikisha watoto 6,417 hii ni sawa na asilimia 48.6 ya lengo.


Na kwa darasa la kwanza walioandikishwa ni 5,882 kati ya matarajio ya kuandikisha watoto 9,397 ikiwa ni sawa na asilimia 62.5 ya maoteo ya uandikishaji.


Aidha, Shiloow amewasihi wazazi na walezi kutoa kipaumbele katika lishe kwa watoto wanapokuwa shuleni kwa  kuchangia gharama za utoaji chakula jambo litakalosaidia kuongeza uelewa darasani kwani lishe hujenga afya ya akili na mwili kwa mtoto.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.