• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

AMEND WASAIDIA KUPUNGUZA AJALI TANGA JIJI

Imewekwa: October 13th, 2023

Naibu Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Rehema Mhina, amelipongeza Shirika lisilo la Serikali, linaloshughulikia usalama barabarani la Amend, kwa kutekeleza mradi wa usalama barabarani maeneo ya shule, uliosaidia kupunguza ajali, hasa kwa watoto na kuwaimarishia usalama wanapotumia barabara.


Mheshimiwa Mhina ametoa pongezi hizo wakati wa hotuba yake ya kufunga rasmi mradi wa usalama wa watoto barabarani uliotekelezwa na shirika la Amend chini ya ufadhili wa Fondation Botnar, katika maeneo ya shule za msingi na sekondari zipatazo kumi na tano (15) kwa kipindi cha miaka minne (2019 - 2023), ikihusisha ujenzi wa vivuko vya waenda kwa miguu, utoaji wa elimu ya matumizi salama ya barabara kwa watoto mashuleni, mafunzo kwa bodaboda na uhamasishaji wa watu kufuata sheria za barabara.


"Jukumu la kuhakikisha usalama wa watoto wetu ni letu sote. Wafadhili wa mradi huu, Botnar na watekelezaji wa mradi, Shirika la Amend, wamefanya mambo ya muhimu katika kutuboreshea miundombinu yetu katika kuhakikisha usalama wa watoto wetu, na  natoa rai kwa watu wote kuendelea kuhamasisha matumizi salama ya barabara" amesisitiza Naibu Meya Mhina.


Naibu Rehema Mhina ametumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuweka mazingira rafiki kwa wafadhili kuleta miradi ya kuwanufaisha wananchi, na kwa nia ya dhati ya kuhakikisha usalama wa watoto pale wanapotumia barabara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shirika la Amend Tanzania, Ndg. Simon Kalolo, amesema barabara salama ni haki ya msingi kwa binadamu wote, lakini watoto wanafaa kupewa upekee zaidi katika safari yao ya kwenda shuleni, na kwamba hawapaswi kuwekwa kwenye hatari ya ajali za barabarani.


Mkutano huo wa kufunga rasmi mradi wa usalama wa watoto barabarani, ulifunguliwa kwa njia ya video na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Alhaj Abdulrahman Shiloow, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo Madiwani, Mwakilishi wa Fondation Botnar, Viongozi kutoka Polisi kikosi cha Usalama barabarani, Walimu na wanafunzi, viongozi wa bodaboda, na wengineo katika usalama barabarani.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.