• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

Kupata kibali cha kwenda nje ya nchi

HATUA ZA KUFUATA

1. SAJILIWA KWENYE MFUMO

Usajili wa kwenye mfumo unafanywa na Afisa TEHAMA wa Halmashauri uliyopo (kama muombaji ni mtumishi wa Halmashauri). Ili usajaliwe yafuatayo yanahitajika:

  1. Majina matatu ya muombaji wa kibali
  2. Namba ya simu ya muombaji wa kibali
  3. Anuani ya barua pepe ya muombaji wa kibali (Inashauriwa kuwa na anuani ya barua pepe ya serikali)
  4. Cheo cha muombaji na Idara anatoka muombaji wa kibali

Afisa TEHAMA atakusajili na kukufundisha namna ya kujaza fomu kwenye mtandao.

 

2. HUISHA AKAUNTI YAKO YA MFUMO

Baada ya kusajiliwa kwenye mfumo, utapokea ujumbe kwenye barua pepe yako (kupitia anuani uliyosajaliwa nayo hapo awali kwenye hatua ya kwanza)

Ujumbe utakupa maelekezo ya namna ya kuingia kwenye mfumo na utakutaka kubadili neno la siri/nywila (password), kisha utaweza kuingia kwenye mfumo na kuanza kufanya maombi ya kibali cha kusafiri nje ya nchi.

MUHIMU: Nywila (password) lazima iwe na sifa neno lenye urefu wa characters nane ambapo ndani yake kuwe na mchanganyiko wa herufi kubwa na ndogo, namba na “special characters - !@$%#” (mfano: Mtanzania123!)

3. INGIA KWENYE MFUMO 

Ukifanikiwa kuingia kwenye mfumo, unatakiwa kubonyeza/kuingia kwenye aneo la “kibali cha safari”. Ili ukamilishe eneo hili, mahitaji yafuatayo lazima yatimizwe;

  1. Kuwa na hati ya kusafiria (passport) na ujue namba yake (passport number)
  2. Fahamu tarehe ya safari (kumbuka: maombi ya kibali yanatakiwa kufanywa siku kumi na nne (14) au zaidi kabla ya tarehe/siku ya safari (kuanza kwa kibali chako). Naombi yatakayofanywa chini ya muda huo hayakubalika kwenye mfumo. Mfano ikiwa zimebaki siku 13 kabla ya tarehe ya safari, maombi yako yatakataliwa na mfumo automatically)
  3. Kama safari inagharamiwa na serikali, fahamu kwa usahihi kiasi cha nauli na posho unayotakiwa kulipwa/kupewa
  4. Utapashwa kutoa melezo juu manufaa ya safari yako kwa taifa (kwa ufupi yasizidi maneno 100)
  5. Kuwa na barua ya mwaliko
  6. Kuwa na barua iliyoidhinishwa na Mkuu wa Idara
  7. Kuwa na barua ya utambulisho kutoka kwa Mkuu wa Taasis yako (kwa halmashauri barua ni ya Mkurugenzi wa halmashauri – Jiji la Tanga)

NOTE:

1: Kama safari ni binafsi kwa matembezi/mapumziko, lazima uwe na barua ya likizo

2: Kama safari ni matibabu ni lazima uwe na vielelezo vinaelezea Ushauri wa Kitabibu na Rufaa ya Matibabu

3: Kama safari ya ni mafunzo ya muda mrefu ni lazima uwe na;

Barua ya Udahili

Barua ya Udhamini wa Masomo

Barua ya Mwaliko

MUHIMU: 

Nyaraka zote hizi ziwe zimefanyiwa scanning kwenye format ya PDF

 

4. KUJAZA FOMU

Mfumo unakuelekeza namna ya kukamilisha kujaza fomu mpaka mwisho. Ukiwa na nyaraka (documents) zilizoanishwa hapo mwanzo, zoezi la kujaza fomu linakuwa fupi. (Melekezo ya jinsi ya kujaza fomu yanatolewa na Afisa TEHAMA aliyekusajili kwenye mfumo)

KUMBUKA: zoezi la kujaza fomu linafanyika kuanzia hatua ya mwanzo hadi ya mwisho kwa wakati mmoja. Maana yake ni kwamba ili uanze kujaza fomu ni lazima uwe na nyaraka zilizotajwa hapo mwanzo.

Mara baada ya kukamilisha ujazaji wa fomu kikamilifu, utawasilisha fomu yako kwa njia hii ya mtandao kwa kubonyeza neno WASILISHA.

Maombi yako yatakuwa yametumwa kwenye mamlaka husika na kufanyiwa kazi (kwa ngazi ya Halmashauri maombi yanatumwa TAMISEMI). Mrejesho wa kibali chako utayapa kwa njia mtandao kama ulivyofanya maombi ya kibali.

 

5: NAMNA YA KUPATA MREJESHO WA MAOMBI

Mrejesho wa maombi unapatikana kwa kuingia kwenye mfumo (kama ulivyoingia wakati wa kuomba kibali), na baada ya kufanikiwa kuingiwa kwenye mfumo, bonyeza/ingia kwenye mrejesho wa safari ili kupata mrejesho. Kipindi cha kupata mrejesho baada ya kuomba kibali inategemea na mamlaka inayohusika na kupitisha vibali.

Kibali kikiwa kipo tayari, unaweza kuprint.

Kuingia kwenye mfumo, bonyeza hapa


kwa maelekezo zaidi tafadhali wasiliana na afisa TEHAMA, au fika ofisi ya kitengo cha TEHAMA - JENGO KUU LA HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA, CHUMBA NA. 18

Matangazo

  • MUDA WA NYONGEZA KULIPA KODI YA PANGO LA ARDHI BILA RIBA February 16, 2023
  • UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI KWA DARASA LA AWALI NA LA KWANZA 2023 December 09, 2022
  • MSAMAHA WA RIBA KWA KODI YA PANGO September 28, 2022
  • MKUTANO MAALUM WA BARAZA LA MADIWANI September 28, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • AKIDAYA WANUFAIKA NA MIKOPO YA HALMASHAURI

    March 22, 2023
  • WAZAZI NA WALIMU KUSHIRIKIANA KUBORESHA ELIMU

    March 22, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI JIJI LAPOKEA RASIMU YA BAJETI 2023/2024

    March 02, 2023
  • KAMATI YA USHAURI WILAYA YAJADILI BAJETI YA BILLION 72.1

    March 02, 2023
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.