• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
Tanga City Council
Tanga City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Usafi wa Mazingira
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jiamii na Vijana
      • Maji
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
    • Kata
    • Mitaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Elimu
    • Sekta ya Viwanda
    • Maeneo ya Nyumba na Makazi
    • Sekta ya Misitu na Mashamba ya Miti
    • Sekta ya Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Uwezeshaji Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Siku za Kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Fomu Mbalimbali
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Majarida
    • Taarifa za Miradi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • TangaTV

HALMASHAURI KUNUNUA VIFAA VYA KISASA VYA KUBEBA TAKATAKA

Imewekwa: December 1st, 2023

Na; Mussa Labani, Tanga.

Halmashauri ya Jiji la Tanga imeendelea kutekeleza jukumu la udhibiti taka zinazozalishwa ili zisilete madhara kwa Jamii, kwa kuhakikisha magari ya uchukuzi taka yanaondoa taka na kuzipeleka dampo, na huku ikiendelea kusajiri vikundi vya taka ni mali vinavyojihusisha na urejerezaji (recycling) taka.


Hivi karibuni, wakati Mwenge wa Uhuru 2023 ulipopita katika Wilaya yetu, moja ya kazi zilizofanywa na Mwenge wa Uhuru, ilikuwa ni pamoja na uzinduzi wa gari jipya la kubeba taka la Halmashauri ya Jiji la Tanga.


Gari hili (pichani) tayari lipo mtaani likiendelea na kazi hiyo, ikiwa ni moja ya mipango ya Halmashauri ya ununuzi wa magari ya kubebea taka ili kurahisisha kazi ya uondoaji wa taka katika mitaa.

Pamoja na ununuzi wa gari hilo, Halmashauri inafanya matengenezo ya vifaa na magari mengine ili kuongeza nguvu katika eneo hilo, huku ikijipanga kununua magari ya kisasa zaidi ya kubeba taka, na kuachana na vifaa vilivyopitwa na wakati.


Jiji la Tanga lina Kata 27, ambazo kwa pamoja zinazalisha zaidi ya Tani 217 za takataka kwa siku. Taka hizi huzalishwa katika kaya, biashara, viwanda, mifugo, n.k.

Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira, Ndg. Kizito Nkwabi anasema, mbali na Jiji kuongeza uwezo wake, lakini pia inashirikisha sekta binafsi, na tayari jambo hilo linafanyika katika Kata za Nguvumali, Pongwe na Maweni.


"Tayari tunawatambua wadhibiti taka 430, ambao hawa ni wadhibiti taka kwa mfumo wa urejerezaji  taka kuwa mali, kuzirudisha taka kwenye mnyororo wa thamani ili zitumike tena kwa manufaa. Hakuna taka ambayo haiwezi kutumika tena." Amesema Ndg. Kizito.


Ili kupata mgawanyo mzuri wa gari za kubeba taka, Halmashauri imekuwa ikitoa ratiba ya magari ya kubeba taka kwa kila kata. Katika hili, Ndugu Kizito anatoa maombi kwa jamii;

"Niwaombe Viongozi na jamii kwa ujumla, kuhakikisha takataka zinawekwa katika vifaa maalum vya kuhifadhia taka, na watoe taka kwa mujibu wa ratiba ya siku ya kupita gari.  Wafuate ratiba ya kupita gari. Lakini pia wasimpe taka mtu asiye rasmi, ambaye hajaidhinishwa na Halmashauri kufanya kazi hiyo. Mfano unampa taka mtu halafu anaziacha mtaa wa pili, hii sio sawa."


Lakini mwisho, Kizito anakumbushia wajibu wa wakazi kulipa huduma hiyo. Hii ni sawa na ule usemi wa 'haki huenda na wajibu'. Tulipe ada ya huduma hii ambayo kwa kaya ni Tsh. 2000 kwa mwezi, huku maeneo ya biashara yakiwa na viwango vyao kwa mujibu wa ukubwa na aina ya biashara.


Kwa pamoja tuweke Jiji letu kuwa safi.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ. March 09, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA JIJI TANGA September 27, 2024
  • TAARIFA YA MSIBA September 18, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 26, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TANGA: MABORESHO DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA FEB. 13, 2025

    February 04, 2025
  • MENEJIMENTI WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI, UMALIZIAJI WA VIPORO.

    February 04, 2025
  • AFUA ZA LISHE ZAFANYA VIZURI TANGA JIJI

    January 24, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI.

    January 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Baraza la Madiwani la kwanza 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matumizi ya TEHAMA kwa Jiji la Tanga
  • Kata na Mitaa ya Jiji la Tanga
  • Manual ya mfumo wa FFARS
  • Muongozo wa ugawaji wa kitambulisho cha mjasiliamali
  • Jarida la Mifumo Yetu - Novemba 2018-Januari 2019
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Tangazo kuhusu watumishi waliomba vibali vya uhamisho
  • Kuanza Ujenzi na Kupata Kibali cha Ujenzi
  • Kuhusu kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi

Tovuti Linganifu

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Mfumo wa Kuomba Vibali vya Nje ya Nchi
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Independent Avenue

    Sanduku la Posta : P.O.BOX 178, Tanga

    Simu ya Mezani: 027 2643068

    Simu ya Mkononi:

    Baruapepe: info@tangacc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Jiji la Tanga . Haki Zote Zimehifadhiwa.